Vito vya Thamarati
Na katika hilo washindane wenye kushindana
Enyi Waislamu: Ni mara ngapi Magharibi imewadanganya baada ya kuharibu dola yenu na mfumo wenu wa kisiasa, na wakafuata walioathiriwa kutoka kwa watoto wenu kwa fikra zao na utamaduni wao mpaka wakaondoa uaminifu kutoka katika vifua vyenu kwamba Uislamu una uwezo wa kutatua matatizo yenu yote na matatizo ya ulimwengu. Sikilizeni, fuateni manhaj ya Mola wenu na fanyeni bidii katika mwendo na kulisha hatua katika kumsimamisha Khalifa na kumpa bay'a juu ya kuhukumu kwa Uislamu na kuunganisha Waislamu wote duniani chini ya bendera ya adhabu.
Enyi Waislamu, enyi watu wa Imani na Hekima: Msidanganyike na fikra za Magharibi zenye kung'aa kwani zimewaangamiza kwa miongo mingi ya miaka, na shindeni katika kumsimamisha Khalifa wa Waislamu ili mpate kushinda kwa utukufu wa dunia na kheri ya Akhera. {Na katika hilo washindane wenye kushindana}
(Enyi mlio amini! Itikieni wito wa Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuiteni kwenye jambo la kukuhuisheni)
Na umsalie, Ewe Mwenyezi Mungu, Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema ya Mwenyezi Mungu na Baraka zake