NAFĀ'ISU ATH-THAMARĀTI
Wosia wa Abu Bakr kwa Omar Radhi za Allah ziwe juu yao
Mauti yalipomfika Abu Bakr As-Siddiq, alimwusia Omar bin Al-Khattab, Radhi za Allah ziwe juu yao, akisema: Ninakuusia wosia, ikiwa utaukubali kutoka kwangu: Hakika Mwenyezi Mungu ana haki ya usiku ambayo haikubali mchana, na hakika Mwenyezi Mungu ana haki ya mchana ambayo haikubali usiku, na hakika hakubali Sunna mpaka itimizwe Fardhi, Je! huoni ewe Omar kwamba mizani iliyo kuwa nzito ni ile iliyo kuwa nzito siku ya Kiyama kwa kufuata kwao haki na uzito wake juu yao, na ni haki kwa mizani ambayo haitawekwa ndani yake kesho ila haki kuwa ni nzito, na hakika mizani iliyo kuwa nyepesi ni ile iliyo kuwa nyepesi katika Akhera kwa kufuata kwao batili, na wepesi wake juu yao katika dunia, na ni haki kwa mizani ambayo itawekwa ndani yake batili kuwa ni nyepesi
Na Rehema za Allah zimshukie Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake