Nafais Althamarati
KATIKA HALI YOYOTE ULIYOPIGANA AU ULIYOUAWA, ALLAH ATAKUFUFUA KATIKA HALI HIYO
Imepokewa kutoka kwa Al-'Alaa bin 'Abdillah bin Raafi', kutoka kwa Hanaan bin Kharija, kutoka kwa 'Abdillah bin 'Amr, amesema: 'Abdillah bin 'Amr amesema: Ewe Mjumbe wa Allah, nieleze kuhusu jihadi na vita, akasema: "Ewe 'Abdillah bin 'Amr, ukipigana kwa subira na kwa kutafuta thawabu, Allah atakufufua ukiwa na subira na unatafuta thawabu, na ukipigana kwa riya na kujionyesha, Allah atakufufua ukiwa unafanya riya na kujionyesha, Ewe 'Abdillah bin 'Amr, katika hali yoyote uliyopigana au uliyouawa, Allah atakufufua katika hali hiyo".
Mola wetu mshushie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote.
Na Amani iwe juu yenu na rehema za Allah na baraka zake