Nafasi za Matunda
KUWA MTU ASIYETARAJIA CHOCHOTE KUTOKA KWA WATU
Kutoka kwa Ubaidillah bin Mihsan Al-Ansari Al-Khatmi Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume wa Allah ﷺ: (Yeyote miongoni mwenu anayeamka akiwa salama katika nafsi yake, na afya katika mwili wake, na ana chakula cha siku yake, basi ni kama vile ulimwengu umekusanywa kwake na vyote vilivyomo).
Na kutoka kwa Saad bin Abi Waqqas Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Alikuja mtu kwa Mtume ﷺ akasema: Ewe Mtume wa Allah, niusie na unifupishie, akasema Mtume ﷺ: (Kuwa mtu asiyetarajia chochote kutoka kwa watu, na tahadhari na tamaa kwani hiyo ni umaskini ulio dhahiri, na tahadhari na jambo ambalo linapelekea kuomba udhuru).
Rehema za Allah ziwe juu ya Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake