Nafasi za Matunda - KUWA MTU ASIYETARAJIA CHOCHOTE KUTOKA KWA WATU
Nafasi za Matunda - KUWA MTU ASIYETARAJIA CHOCHOTE KUTOKA KWA WATU

 

0:00 0:00
Speed:
July 13, 2025

Nafasi za Matunda - KUWA MTU ASIYETARAJIA CHOCHOTE KUTOKA KWA WATU

Nafasi za Matunda

KUWA MTU ASIYETARAJIA CHOCHOTE KUTOKA KWA WATU

Kutoka kwa Ubaidillah bin Mihsan Al-Ansari Al-Khatmi Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume wa Allah ﷺ: (Yeyote miongoni mwenu anayeamka akiwa salama katika nafsi yake, na afya katika mwili wake, na ana chakula cha siku yake, basi ni kama vile ulimwengu umekusanywa kwake na vyote vilivyomo). 

Na kutoka kwa Saad bin Abi Waqqas Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Alikuja mtu kwa Mtume ﷺ akasema: Ewe Mtume wa Allah, niusie na unifupishie, akasema Mtume ﷺ: (Kuwa mtu asiyetarajia chochote kutoka kwa watu, na tahadhari na tamaa kwani hiyo ni umaskini ulio dhahiri, na tahadhari na jambo ambalo linapelekea kuomba udhuru).

Rehema za Allah ziwe juu ya Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake

More from null

Thamani za Matunda - Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Thmani za Matunda

Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Alisema Al-Hasan Al-Basri, Mwenyezi Mungu amrehemu: Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea, na Kiyama ndio ahadi yake, na kusimama mbele ya Mwenye Nguvu, ndio mahali pake pa kushuhudia, huzuni yake iwe ndefu duniani, na hamu yake iwe katika matendo mema. 

Adabu za Al-Hasan Al-Basri, kujiepusha kwake na dunia na mawaidha yake

Na Abu al-Faraj Ibn al-Jawzi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake

Zawadi Bora - Kukamilisha Kazi Mara Moja

Zawadi Bora

Kukamilisha Kazi Mara Moja

Miongoni mwa mambo yenye manufaa ni kukamilisha kazi mara moja, na kuwa na muda wa ziada katika siku zijazo kwa sababu kazi zisipokamilishwa, mabaki ya kazi zilizopita yatakusanyika, na kazi za baadaye zitaongezeka, na uzito wake utaongezeka, lakini ukikamilisha kila kitu kwa wakati wake, utafanya mambo yajayo kwa nguvu ya mawazo na nguvu ya kazi. 

Njia za Kufurahia Maisha kwa Furaha

Na Ibn Saadi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad, ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake