Nafaisi Althamarati
Sura ya Kuthamini Matokeo
Mwenye kuona kwa jicho la busara mwisho wa mambo katika mianzo yake, hupata kheri yake, na huokoka na shari yake.
Na asiyeona matokeo hushindwa na hisia, hivyo humrudia kwa uchungu yale aliyo yataka ya salama na kwa taabu yale aliyo yatarajia ya raha.
Na ufafanuzi wa haya uko katika mustakabali, utabainika kwa kutaja yaliyopita, nayo ni kwamba wewe huachi, kuwa umemuasi Mungu katika umri wako, au umemtii.
Basi iko wapi ladha ya uasi wako? Na iko wapi taabu ya utiifu wako? Hayawi hayawi kila mmoja ameenda na yaliyomo! Laiti madhambi yalipo achana yangeacha! Na nakuzidishia katika hili ufafanuzi: mfano wa saa ya mauti, na angalia machungu ya majuto juu ya upotevu, na sisemi: vipi utamu wa ladha unashinda, kwa sababu utamu wa ladha umegeuka kuwa handharah, hivyo umebaki uchungu wa huzuni bila pingamizi.
Je! huoni kwamba jambo liko na matokeo yake? Basi chunga matokeo utasalimika, wala usifuate matamanio ya hisia ukajuta.
Swidi Alkhatiri
Ibn Aljawzi
Mola Amsali Mtume wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh