Nafasi za Matunda
Ghanima ya Akhera Katika Mambo Matatu
Amesema Yahya bin Muadh, Allah amrehemu: Ewe mwanaadamu umeitafuta dunia kama kwamba huna budi nayo, na umeitafuta Akhera kama kwamba huna haja nayo, na dunia umekwisha kutoshelezwa nayo hata kama hukuitafuta, na Akhera kwa kuitafuta kwako utaipata basi fahamu jambo lako.
Na amesema Allah amrehemu: Ghanima ya Akhera katika mambo matatu: utiifu, wema na uasi. Utiifu kwa Mola, na wema kwa wazazi, na uasi kwa shetani.
Mola wasalia Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh