Nafaisi Al-Thamarat
Moto Umharamishiwa Jicho Lililotoa Machozi kwa Kumcha Mwenyezi Mungu
Kutoka kwa Abi Rayhana Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Tulitoka na Mtume wa Allah rehema na amani zimshukie katika vita, nikamsikia akisema: "Moto umeharamishwa kwa jicho lililotoa machozi kwa kumcha Mwenyezi Mungu, moto umeharamishwa kwa jicho lililokesha katika njia ya Mwenyezi Mungu, na nimesahau ya tatu na nilisikia baadaye kwamba alisema moto umeharamishwa kwa jicho lililoacha kutazama yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu" Ameipokea Ahmad na Al-Hakim na wameisahihisha na wameafikiana na Al-Dhahabi na Al-Nisai na matamshi ni ya Al-Nisai.
Mwenyezi Mungu amrehemu Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake