Nafaisi Al-Thamarat - Moto Umharamishiwa Jicho Lililotoa Machozi kwa Kumcha Mwenyezi Mungu
Nafaisi Al-Thamarat - Moto Umharamishiwa Jicho Lililotoa Machozi kwa Kumcha Mwenyezi Mungu

Kutoka kwa Abi Rayhana Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Tulitoka na Mtume wa Allah rehema na amani zimshukie katika vita, nikamsikia akisema: "Moto umeharamishwa kwa jicho lililotoa machozi kwa kumcha Mwenyezi Mungu, moto umeharamishwa kwa jicho lililokesha katika njia ya Mwenyezi Mungu, na nimesahau ya tatu na nilisikia baadaye kwamba alisema moto umeharamishwa kwa jicho lililoacha kutazama yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu" Ameipokea Ahmad na Al-Hakim na wameisahihisha na wameafikiana na Al-Dhahabi na Al-Nisai na matamshi ni ya Al-Nisai.

0:00 0:00
Speed:
November 08, 2025

Nafaisi Al-Thamarat - Moto Umharamishiwa Jicho Lililotoa Machozi kwa Kumcha Mwenyezi Mungu

Nafaisi Al-Thamarat

Moto Umharamishiwa Jicho Lililotoa Machozi kwa Kumcha Mwenyezi Mungu

Kutoka kwa Abi Rayhana Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Tulitoka na Mtume wa Allah rehema na amani zimshukie katika vita, nikamsikia akisema: "Moto umeharamishwa kwa jicho lililotoa machozi kwa kumcha Mwenyezi Mungu, moto umeharamishwa kwa jicho lililokesha katika njia ya Mwenyezi Mungu, na nimesahau ya tatu na nilisikia baadaye kwamba alisema moto umeharamishwa kwa jicho lililoacha kutazama yale aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu" Ameipokea Ahmad na Al-Hakim na wameisahihisha na wameafikiana na Al-Dhahabi na Al-Nisai na matamshi ni ya Al-Nisai. 

Mwenyezi Mungu amrehemu Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake

More from null

Thamani za Matunda - Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Thmani za Matunda

Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Alisema Al-Hasan Al-Basri, Mwenyezi Mungu amrehemu: Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea, na Kiyama ndio ahadi yake, na kusimama mbele ya Mwenye Nguvu, ndio mahali pake pa kushuhudia, huzuni yake iwe ndefu duniani, na hamu yake iwe katika matendo mema. 

Adabu za Al-Hasan Al-Basri, kujiepusha kwake na dunia na mawaidha yake

Na Abu al-Faraj Ibn al-Jawzi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake

Zawadi Bora - Kukamilisha Kazi Mara Moja

Zawadi Bora

Kukamilisha Kazi Mara Moja

Miongoni mwa mambo yenye manufaa ni kukamilisha kazi mara moja, na kuwa na muda wa ziada katika siku zijazo kwa sababu kazi zisipokamilishwa, mabaki ya kazi zilizopita yatakusanyika, na kazi za baadaye zitaongezeka, na uzito wake utaongezeka, lakini ukikamilisha kila kitu kwa wakati wake, utafanya mambo yajayo kwa nguvu ya mawazo na nguvu ya kazi. 

Njia za Kufurahia Maisha kwa Furaha

Na Ibn Saadi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad, ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake