Vito Vya Matunda
Wanachoogopa Amerika, Taifa la Kiyahudi na Mataifa ya Magharibi
Enyi Waislamu:
Jambo ambalo Amerika, Taifa la Kiyahudi na mataifa yote ya Magharibi wanaliogopa zaidi ni nyinyi kurejea kwenye Uislamu wenu na kuwezesha kikamilifu sheria ya Mola wenu katika dola ya Kiislamu ambayo ni dola ya Khilafa, ili muishi maisha sahihi ya Kiislamu, na wanachoogopa zaidi ni kwenu kusimamisha dola hii kati ya mataifa, ili muanze na da'wa na jihad kuikomboa watu wa dunia kutoka kwa kuabudu waja, manufaa na ubepari wa kilimwengu hadi kumwabudu Mwenyezi Mungu Mmoja Mwenye nguvu, na kuwatoa katika dhiki ya dunia hadi wasaa wa dunia na Akhera, na kutoka katika dhulma ya dini hadi uadilifu wa Uislamu, na watu hawa wanawasubiri nyinyi kama wao ili kuwaokoa kutoka kwa dhulma na ukandamizaji ambao wako chini yake, na hii ndio kazi ambayo Mwenyezi Mungu amewakabidhi na amewaandaa kwa ajili yake kama umma wa Kiislamu, na Mwenyezi Mungu atatuuliza Siku ya Kiyama kuhusu watu hawa na ujumbe huo, je, tuliwapelekea? Mwenyezi Mungu anasema: (Na hivyo tumekufanyeni umma wa wastani ili muwe mashahidi kwa watu, na Mtume awe shahidi juu yenu).
Rehema na amani zimshukie Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh