Vito Vizuri
Sina Shida na Dunia
Kutoka kwa Abdallah bin Masoud, Radhi za Allah ziwe juu yake, amesema: Mtume wa Allah, Rehema na Amani zimshukie, alilala juu ya mkeka, akaamka na ulikuwa umemwathiri ubavuni mwake, tukasema: Ewe Mtume wa Allah, lau tungekufanyia kitanda laini, akasema: (Sina shida na dunia, mimi si chochote katika dunia isipokuwa kama mpanda farasi aliyepumzika chini ya mti kisha akaenda na kuuacha).
Mola wetu Mlezi mfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba wake wote.
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake