Vito Vya Thamarati
Pale Unapojiona Umelema
Na pale unapoona ulemavu ndani yako basi muombe Mwenye Kuneemesha, au uvivu basi mkimbilie Mwenye Kufanikisha, hutapata kheri ila kwa kumtii, wala haitakupita kheri ila kwa kumuasi, na nani yule aliyemuelekea asione kila alichokitaka kwake? Na nani aliyempa mgongo akaenda na faida? Au akapata lengo katika malengo yake?
Au hukusikia usemi wa mshairi:
Usiku sikukuijieni nikiwa mgeni ila ... niliona ardhi ikikunjwa kwa ajili yangu
Wala sikukunjua azma yangu kutoka mlangoni mwenu ... ila niliyumbishwa na nguo zangu ndefu
Kitabu: Lile Pigo la Ini katika Ushauri kwa Mwana
Cha Imamu Ibn Al-Jawzi akimusia mwanawe ndani yake
Mola wasalia juu ya Bwana wetu Muhammad na jamaa zake na masahaba wake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake