Zawadi Bora - WALAHA HATAMJAALIA ALLAH KAFIRI JUU YA MUUMINI NJIA
Zawadi Bora - WALAHA HATAMJAALIA ALLAH KAFIRI JUU YA MUUMINI NJIA

Hakika kusimamisha Khilafa juu ya njia ya Utume kama alivyotoa bishara kwayo Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم, kunahitaji kwanza kuwa mamlaka ya Umma ni ya asili; na ili mamlaka ya Umma iwe ya asili ni lazima ifanye kazi kwa uwezo wake wa asili, na juhudi zake za asili, ikitumia uwezekano wake wa asili, ikimtegemea Mwenyezi Mungu pekee Subhaanahu,

0:00 0:00
Speed:
October 21, 2025

Zawadi Bora - WALAHA HATAMJAALIA ALLAH KAFIRI JUU YA MUUMINI NJIA

Zawadi Bora

WALAHA HATAMJAALIA ALLAH KAFIRI JUU YA MUUMINI NJIA

Hakika kusimamisha Khilafa juu ya njia ya Utume kama alivyotoa bishara kwayo Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم, kunahitaji kwanza kuwa mamlaka ya Umma ni ya asili; na ili mamlaka ya Umma iwe ya asili ni lazima ifanye kazi kwa uwezo wake wa asili, na juhudi zake za asili, ikitumia uwezekano wake wa asili, ikimtegemea Mwenyezi Mungu pekee Subhaanahu, Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (NA JUU YA ALLAH NA WATEGEMEE WAUMINI); ili iweze kuondokana na ushawishi wa kafiri (Amerika, Urusi, Uingereza, Ufaransa na kila dola yenye tamaa na nchi za Waislamu), Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: (WALAHA HATAMJAALIA ALLAH KAFIRI JUU YA MUUMINI NJIA) Basi pindi mamlaka ya Umma itakapo kuwa ya asili itakuwa na uwezo wa kuamua hatma yake na kutekeleza matakwa yake na kutekeleza kitabu cha Mola wake na kusimamisha Khilafa yake.

{ENYI MLIO AMINI! MUITIKIENI ALLAH NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYOKUHUSHENI, NA MJUE YA KWAMBA ALLAH HINGILIA BAINA YA MTU NA MOYO WAKE, NA YA KWAMBA KWAKE YEYE MTAFUSHWA * NA ILINDENI FITNA ISIWAFIKIE PEKEE WALE WALIO DHULUMU MIONGONI MWENU, NA MJUE YA KWAMBA ALLAH NI MKALI WA ADHABU}

Na Rehema za Allah zimfikie Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Allah na Baraka zake



More from null

Thamani za Matunda - Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Thmani za Matunda

Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Alisema Al-Hasan Al-Basri, Mwenyezi Mungu amrehemu: Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea, na Kiyama ndio ahadi yake, na kusimama mbele ya Mwenye Nguvu, ndio mahali pake pa kushuhudia, huzuni yake iwe ndefu duniani, na hamu yake iwe katika matendo mema. 

Adabu za Al-Hasan Al-Basri, kujiepusha kwake na dunia na mawaidha yake

Na Abu al-Faraj Ibn al-Jawzi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake

Zawadi Bora - Kukamilisha Kazi Mara Moja

Zawadi Bora

Kukamilisha Kazi Mara Moja

Miongoni mwa mambo yenye manufaa ni kukamilisha kazi mara moja, na kuwa na muda wa ziada katika siku zijazo kwa sababu kazi zisipokamilishwa, mabaki ya kazi zilizopita yatakusanyika, na kazi za baadaye zitaongezeka, na uzito wake utaongezeka, lakini ukikamilisha kila kitu kwa wakati wake, utafanya mambo yajayo kwa nguvu ya mawazo na nguvu ya kazi. 

Njia za Kufurahia Maisha kwa Furaha

Na Ibn Saadi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad, ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake