Nafaisi Al-Thamarat - Enyi mlio amini, mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu
Nafaisi Al-Thamarat - Enyi mlio amini, mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu

Enyi Waislamu,

0:00 0:00
Speed:
October 24, 2025

Nafaisi Al-Thamarat - Enyi mlio amini, mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu

Nafaisi Al-Thamarat

Enyi mlio amini, mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu

Enyi Waislamu,

Hakuna wokovu kwenu ila kwa Uislamu, na dhuluma haitaondolewa kwenu ila kwa kutekeleza sheria ya Mwenyezi Mungu, mmekwisha jaribu ujamaa na ubepari na utaifa na uzalendo, na hali ya watu iko katika kuzorota katika kila nyanja za maisha, basi katupeni bendera za Sykes-Picot, na inueni bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم, na fanyeni kazi na Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha sheria ya Mwenyezi Mungu kupitia dola ya Khilafah ya Kiislamu iliyoongoka ambayo ndiyo pekee ina wokovu wenu, na Mwenyezi Mungu yuko pamoja nanyi na hatopunguza thawabu za amali zenu.

(Enyi mlio amini, mkimnusuru Mwenyezi Mungu, naye atakunusuruni na atathibitisha nyayo zenu)  

Na rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu ya Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake

More from null

Thamani za Matunda - Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Thmani za Matunda

Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea

Alisema Al-Hasan Al-Basri, Mwenyezi Mungu amrehemu: Ni haki kwa yule anayejua kwamba mauti ndio mahali pake pa kuelekea, na Kiyama ndio ahadi yake, na kusimama mbele ya Mwenye Nguvu, ndio mahali pake pa kushuhudia, huzuni yake iwe ndefu duniani, na hamu yake iwe katika matendo mema. 

Adabu za Al-Hasan Al-Basri, kujiepusha kwake na dunia na mawaidha yake

Na Abu al-Faraj Ibn al-Jawzi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mwenyezi Mungu na baraka zake

Zawadi Bora - Kukamilisha Kazi Mara Moja

Zawadi Bora

Kukamilisha Kazi Mara Moja

Miongoni mwa mambo yenye manufaa ni kukamilisha kazi mara moja, na kuwa na muda wa ziada katika siku zijazo kwa sababu kazi zisipokamilishwa, mabaki ya kazi zilizopita yatakusanyika, na kazi za baadaye zitaongezeka, na uzito wake utaongezeka, lakini ukikamilisha kila kitu kwa wakati wake, utafanya mambo yajayo kwa nguvu ya mawazo na nguvu ya kazi. 

Njia za Kufurahia Maisha kwa Furaha

Na Ibn Saadi

Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad, ahli zake na masahaba zake wote

Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake