Vito Vya Matunda
ENYI WATU WETU, ITIKIENI MWENYE KUITIA KWA ALLAH
Enyi Waislamu
Hakika mmekwishajaribu kwa miongo kadhaa uongo na hila za mifumo yenu, ambayo ufisadi wake umewafika watu wote na kuwa gumzo la watoto na wakubwa, je! haijawadia kwenu kusimama na mifumo hii msimamo ambao unamridhisha Mola wenu na kuhifadhi dini yenu, na utume ujumbe wa wazi kwa watawala kwamba ikiwa wao wanaendelea katika ghadhabu za Mwenyezi Mungu ili wapate radhi za Magharibi makafiri, basi waende peke yao, kwa sababu hamtomkasirisha Mwenyezi Mungu kwa radhi ya yeyote katika viumbe vyake.
Hakika sisi katika Hizb ut-Tahrir tunakuiteni kwa yale ambayo ndani yake kuna utukufu wenu na ukombozi wenu na utiifu kwa Mola wenu, tunakuiteni kukataa mifumo yote ya kikafiri na kurudi kwenye sheria ya Mwenyezi Mungu kwa kufanya kazi na Hizb ut-Tahrir ili kusimamisha dola ya Khilafah kwa njia ya Utume ambayo ni ahadi ya Mola wenu na bishara ya Nabii wenu Mtukufu, na njama ya adui yenu, na njia yenu ya kupata utukufu wa dunia na thawabu za Akhera.
﴿ENYI WATU WETU, ITIKIENI MWENYE KUITIA KWA ALLAH NA MUAMINI YEYE ATAKUSAMEHEENI DHAMBI ZENU NA ATAKULINDENI NA ADHABU IUMIZAYO * NA YULE ASIYEMUITIKIA MWENYE KUITIA KWA ALLAH BASI HAWEZI KUMSHINDA ALLAH KATIKA ARDHI WALA HAWEZI KUWA NA WALINZI BADALA YAKE HAO WAMO KATIKA UPUZI ULIO WAZI﴾
Rehema za Mwenyezi Mungu zimshukie Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mwenyezi Mungu na Baraka zake