Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Watu wa Al-Fashir Kati ya Nyundo ya Vita na Kipalo cha Njaa, na Hawana Ukombozi Ila kwa Dola ya Khilafa

Watu wa Al-Fashir Kati ya Nyundo ya Vita na Kipalo cha Njaa, na Hawana Ukombozi Ila kwa Dola ya Khilafa

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na mapigano kati ya pande zinazopigana, ambapo raia kadhaa wameuawa katika siku chache zilizopita, wakati wakazi wanakabiliwa na mzingiro mkali, kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, huku kukiwa na ukimya wa kimataifa wa kutiliwa shaka, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha kuuawa kwa watu wasiopungua 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Mwisho wa uvamizi wa kijeshi wa Marekani na Jumuiya ya kujihami ya NATO ni fursa ya kukabiliana na ukoloni mambo leo laini na kuelekea kwenye Ukhalifa kwa mfumo wa Utume!

Mwisho wa uvamizi wa kijeshi wa Marekani na Jumuiya ya kujihami ya NATO ni fursa ya kukabiliana na ukoloni mambo leo laini na kuelekea kwenye Ukhalifa kwa mfumo wa Utume!

Miaka minne iliyopita, tarehe 31 Agosti 2021, uvamizi wa kijeshi wa Marekani na vikosi vya Jumuiya ya kujihami ya NATO (NATO) nchini Afghanistan, ambao ulidumu kwa miongo miwili, uliisha kwa kuondoka kwa askari wa mwisho wa Marekani kutoka humo saa sita za usiku. Hii inatokana hasa na mabadiliko ya lengo la Marekani kuelekea eneo la Bahari ya Hindi na Pasifiki, ili kupunguza kasi ya maendeleo ya China. Nchi ya Kiislamu, hasa Afghanistan na watu wake wanamgambo, imekuwa chanzo cha usumbufu kwa Marekani, na chanzo cha kukengeusha fikira zake kutoka kwa mkakati huu mpya. Tunabariki na tunaendelea kubariki mafanikio haya ya kihistoria na siku hii kuu kwa Waislamu wote, hasa watu wa Afghanistan, kampeni ya Da'wah, na wanamgambo.

135 / 10603