Rada: Taarifa kwa Vyombo vya Habari kutoka Hizb ut-Tahrir Wilaya ya Sudan Enyi watu wa Sudan, mna uwezo wa kufelisha mpango wa kuikata Darfur, basi simameni kwa utiifu kwa Mwenyezi Mungu!
Katika hatua iliyotarajiwa, kiongozi wa vikosi vya usaidizi wa haraka, Muhammad Hamdan Daglo, aliapa kama rais wa baraza la urais la kile kinachoitwa serikali sambamba, katika Nyala, mji mkuu wa kusini mwa Darfur, Jumamosi, 30/8/2025, na vile vile naibu rais, wajumbe wa baraza la urais, na waziri mkuu walikula kiapo. Hatua hii ilitarajiwa kama sehemu ya mpango wa uhalifu wa Amerika, unaolenga kuitenganisha Darfur, kupitia vibaraka wake kutoka kwa viongozi wa jeshi, viongozi wa vikosi vya usaidizi wa haraka, na mamluki wa siasa.