Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Jarida la Al-Raya: Taasisi ya Kiyahudi na Ujumuishaji wa Ukingo wa Magharibi na Kulazimisha Utawala

Jarida la Al-Raya: Taasisi ya Kiyahudi na Ujumuishaji wa Ukingo wa Magharibi na Kulazimisha Utawala

Mipango ya Wayahudi ya kuunganisha Ukingo wa Magharibi na kulazimisha mamlaka juu yake si jambo jipya wala maneno ya kupita, bali ni mipango iliyoingia katika akili na dhamiri za Wayahudi tangu walipoipora Palestina mwaka 1948 BK. Na wameiweka katika utekelezaji wa kivitendo ardhini baada ya kunyakua Ukingo wa Magharibi kufuatia mchezo wa vita vya Juni mwaka 1967 BK. Ni muhimu katika muktadha huu kukagua muhtasari wa kihistoria wa mkondo wa matukio haswa tangu mwaka 1947 BK,

Jarida la Ar-Raya: Kwa nini Urusi ilitambua serikali ya Taliban?

Jarida la Ar-Raya: Kwa nini Urusi ilitambua serikali ya Taliban?

Urusi imetambua rasmi Imarati ya Kiislamu ya Afghanistan, kama ilivyoripotiwa na shirika la habari la TASS likimnukuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi. Kulingana na shirika hilo, bendera ya Afghanistan iliyopitishwa na Taliban ilipandishwa juu ya ubalozi huko Moscow. Kulingana na balozi wa Urusi huko Kabul, Dmitry Zhirnov, Putin alichukua uamuzi huu wa kutambua kulingana na pendekezo kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov. Kulingana na mwanadiplomasia huyo, uamuzi huo "unaonyesha nia ya dhati ya Urusi ya kuanzisha ushirikiano kamili na Afghanistan."

Jarida la Ar-Raya: Bwawa la Renaissance ni uhalifu mpya unaoanika ulegevu na usaliti wa mfumo wa Misri

Jarida la Ar-Raya: Bwawa la Renaissance ni uhalifu mpya unaoanika ulegevu na usaliti wa mfumo wa Misri

Kituo cha Al Arabiya kilichapisha kwenye tovuti yake Alhamisi, 2025/7/3, chini ya kichwa "Misri kwa Ethiopia: Ufunguzi wa Bwawa la Renaissance si halali na unakiuka sheria za kimataifa," habari ambayo ilisema: Waziri wa Umwagiliaji wa Misri Hani Sweilem alisisitiza kukataa kwa Cairo sera ya kulazimisha hali halisi kupitia hatua za upande mmoja bila makubaliano ya lazima ambayo yanazingatia maslahi ya Misri na Sudan, akishutumu Ethiopia kwa kukosa utashi wa kisiasa na ujanja wa kukuza picha chanya licha ya kukwama kwa mazungumzo kwa miaka 13. Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Ethiopia alidai kuwa bwawa hilo halijaathiri akiba ya maji ya Misri au Sudan, wakati Misri ilisisitiza kwamba faili hii ni suala la kuishi na haitaruhusu kulazimisha utawala wa maji.

Jarida la Al-Raya: Marekani yatangaza kuanza vikwazo dhidi ya Sudan - Maoni na Matokeo Yake

Jarida la Al-Raya: Marekani yatangaza kuanza vikwazo dhidi ya Sudan - Maoni na Matokeo Yake

Tovuti ya Sudan Tribune iliripoti mnamo Juni 26 kwamba utawala wa Marekani ulitangaza, siku ya Alhamisi, kuanza kutekeleza vikwazo dhidi ya Sudan, kufuatia kuishtaki kwa kutumia silaha za kemikali wakati wa vita vyake dhidi ya Vikosi vya Msaada wa Haraka, vilivyoanza nchini humo katikati ya Aprili 2023. Mnamo Mei 22, 2025, Marekani iliweka vikwazo dhidi ya Sudan, ikiwa ni pamoja na vizuizi vya mauzo ya bidhaa za Marekani kwenda Sudan na upatikanaji wa laini za mikopo, lakini vikwazo vilianza kutekelezwa rasmi kuanzia Alhamisi, Juni 26, 2025.

Jarida la Ar-Raya: ﴿WALA MSIZOZANE MTAFUTIKA NA UONDOKE UPEPO WENU﴾

Jarida la Ar-Raya: ﴿WALA MSIZOZANE MTAFUTIKA NA UONDOKE UPEPO WENU﴾

Hakika mataifa hayasimami wala hayawezi kuwa na nguvu, isipokuwa kwa umoja unaowaunganisha watu wake, na umoja huu ndio itikadi, ambayo huamua mfumo unaowatawala, na huelekeza njia yao. Itikadi ikishikamana, na mfumo ukaandaliwa, msimamo wa umma huungana, na unakuwa kama mwili mmoja unaosonga kwa mapigo moja, nguvu za watu binafsi hubadilika na kuwa nguvu ya pamoja yenye nguvu, kama upepo mkali ambao hakuna kinachosimama mbele yake.

Jarida la Ar-Raya: Mkutano wa Shirika la Shanghai Nchini China Haukuleta Jambo Jipya

Jarida la Ar-Raya: Mkutano wa Shirika la Shanghai Nchini China Haukuleta Jambo Jipya

Mnamo Alhamisi, 2025/6/26, mkutano wa mawaziri wa ulinzi wa nchi wanachama wa Shirika la Ushirikiano la Shanghai ulifanyika katika jiji la Qingdao nchini China. Mkutano huo uliongozwa na Waziri wa Ulinzi wa China, Dong Jun, ambaye alitoa hotuba akihudhuriwa na mawaziri wa ulinzi walioshiriki na kusema: "Ulimwengu unashuhudia mabadiliko ambayo hayajawahi kushuhudiwa chini ya kuongezeka kwa utawala," na akaelezea mkutano huo kama "kipimo cha uzani katika ulimwengu ambapo machafuko na mabadiliko yanaingiliana," na akasema kwamba "ulimwengu unashuhudia mabadiliko ambayo hayajawahi kushuhudiwa kwa karne moja chini ya kuongezeka kwa upande mmoja, ulinzi, na mazoea ya utawala na uonevu ambayo yanatishia mfumo wa kimataifa na kuunda hali ya ukosefu wa utulivu,"

218 / 10603