Jarida la Ar-Raya: Pakistan Lazima Itambue Ukubwa wa Nguvu Zake Ili Kujiweka Huru Kutoka Utawala wa Kimarekani na Kihindi (Kimetafsiriwa)
Tangu kusitishwa kwa mapigano kulikosimamiwa na Rais wa Marekani Donald Trump, Pakistan imeonyesha hamu kubwa ya kuanzisha mazungumzo ya kina na India kuhusu masuala kadhaa ya kiusalama, ikiwa ni pamoja na mustakabali wa Kashmir, kupunguza mivutano kwenye mstari wa udhibiti, na muhimu zaidi, kubatilisha uamuzi wa India wa kusitisha mkataba wa maji wa Indus, kwani mkataba huu unaipatia Pakistan takriban 80% ya mahitaji yake ya maji kutoka mito mitatu mikuu ambayo ni: Indus, Chenab, na Ravi.