Jarida la Ar-Raya: Msafara wa Msimamo Imara Kati ya Ushawishi wa Utawala wa Misri na Ulazima wa Jeshi Lake Kuchukua Hatua
Wakati viongozi wa tawala za Kiarabu wanaadhimisha mikutano mitupu na makongamano ya udanganyifu, msafara wa wananchi uliojiita "Msafara wa Msimamo Imara", ulitoka Tunisia, Algeria, na Morocco kuelekea Gaza kupitia Libya na Misri, kwa lengo la kuvunja mzingiro na kuunga mkono watu wa Ukanda uliyo mzingirwa kwa zaidi ya miezi 18. Msafara huo ulibeba wanaume na wanawake wa rika tofauti, waliokusanyika kwa lengo moja la kuvunja mzingiro huu unaowekwa na shirika la Kiyahudi kwa watu wa Gaza, kwa ushirikiano na ushiriki wa moja kwa moja wa tawala za jirani, hasa utawala wa Misri.