Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Kuhamasisha Watu Wenye Nia ya Kufanya Wajibu Wao

Kuhamasisha Watu Wenye Nia ya Kufanya Wajibu Wao

Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA TUMEKUTEREMSHIA KITABU KIELEZO CHA KILA KITU﴾, basi ubainifu huu wa Kiungu unasisitiza kuwa Uislamu si mawaidha tu ya kiroho, bali ni mfumo kamili wa maisha, umekuja na itikadi thabiti inayoshawishi akili na kujaza moyo utulivu, na kwa hukumu zinazoongoza maisha ya mwanadamu katika mambo yake yote: katika utawala, uchumi, jamii, siasa, elimu na uhusiano wa kimataifa... Hakika hii ni dini ya haki, kwa sababu inatoka kwa Mwenyezi Mungu, na imejengwa juu ya msingi imara, nayo ni itikadi ya Kiislamu ambayo mfumo hutokana nayo, hivyo basi uhusiano wa mwanadamu nayo unakuwa ni wa kiakili kwa ushawishi, siyo kwa kufuata wala hisia, basi inakubaliana na fitra njema na inazungumza na akili, na kwa hivyo anayemwamini kwa imani timamu hawezi ila kuubeba na kuulingania na kupigania kuudhihirisha na kuutekeleza,

Watawala wa Kiislamu Hawafai Kuhifadhi Heshima za Waislamu!

Watawala wa Kiislamu Hawafai Kuhifadhi Heshima za Waislamu!

Vyombo vya habari vimeeneza habari za rais wa Marekani Donald Trump akicheza dansi kwenye zulia jekundu katika uwanja wa ndege nchini Malaysia alipokuwa akipokelewa na waziri mkuu wa Malaysia siku ya Jumapili 2025/10/26, na alikuwa amewakusanya idadi ya watu wa Malaysia, wanaume na wanawake, wakipeperusha bendera za Marekani na kucheza dansi kwa nyimbo za kienyeji kumkaribisha muuaji mhalifu ambaye mikono yake imetiwa damu ya Waislamu huko Gaza.

38 / 10603