Kuondolewa kwa Waziri Mkuu wa Malaysia Bila Uchaguzi Mkuu Sio Suluhisho la Kweli Uislamu Pekee Ndio Suluhisho la Matatizo ya Umma
Mnamo Julai 26, 2025, Malaysia ilishuhudia maandamano makubwa yakitaka kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Datuk Seri Anwar Ibrahim. Waandamanaji hao walishirikisha wafuasi wa upinzani, mashirika yasiyo ya kiserikali, na watu wa kawaida waliokasirishwa na kile walichokiona kama kushindwa kwa uongozi. Wengi walieleza imani yao kwamba Anwar Ibrahim anahusika na kuzidisha matatizo yanayowakabili watu. Wakati baadhi walibishana kwamba Waziri Mkuu anaweza kubadilishwa tu kupitia uchaguzi, Waziri Mkuu wa zamani Dk. Mahathir Mohammed alisisitiza kwamba Waziri Mkuu yeyote anaweza kuondolewa madarakani bila kusubiri uchaguzi mkuu. Matamshi yake yalizua mjadala mkubwa, na kuzidisha migawanyiko ya kisiasa kati ya wafuasi wa serikali na upinzani.