
2025-08-11
Rada: Profesa/Um Suhaib Anaandika.. Sudan: Janga la Karne Lililo Fichika Machoni pa Dunia
Dola ya Kiislamu iliyokuwa inawalinda raia wake imetoweka, na Waislamu wanaishi katika dhiki, mateso na majanga kote ulimwenguni, ikiwa ni pamoja na Sudan, ambayo hivi sasa inakabiliwa na mojawapo ya majanga mabaya zaidi ya kibinadamu katika historia ya hivi karibuni kutokana na mapigano ya umwagaji damu ambayo yanaendelea kwa miaka miwili kati ya jeshi na vikosi vya msaada wa haraka, ambayo yamesababisha majanga ya kutisha ambayo hakuna mtu anayeongelea au kujaribu kuyaondoa. Mapigano yaliyosahaulika ambayo vyombo vya habari havitoi mwanga na hakuna nchi au taasisi zinazofichua mambo yake ya ndani.
Wakazi wanateseka kwa ukiukwaji mkubwa unaojumuisha mauaji ya halaiki, uhamishaji, ukimbizi wa kulazimishwa, njaa, magonjwa, unyanyasaji wa kijinsia na majanga mengine, na hakuna mwangalizi wala msimamizi!
Huku ukatili ukitendwa na pande zote mbili zinazopigana, makadirio yanaonyesha idadi ya kushtua ya vifo na majeruhi, haswa miongoni mwa wanawake, watoto na wazee, na idadi ya vifo inakadiriwa kuwa si chini ya watu 150,000, ambao zaidi ya 60,000 wao wakiwa katika jimbo la Khartoum pekee katika miezi 14 ya kwanza ya mzozo.
Idadi ya majeruhi imezidi watu 70,000, huku kukiwa na matatizo makubwa katika kupata huduma za matibabu kutokana na kuporomoka kwa mfumo wa afya na kusitishwa kwa kazi kwa 70-80% ya taasisi za afya, na kuenea kwa magonjwa kama vile kipindupindu, surua na kuhara. Vile vile, elimu imeporomoka; kuna takriban watoto milioni 20 nchini Sudan leo ambao hawaendi shule.
Maeneo mengi yameshuhudia mauaji ya kutisha, mauaji ya kikatili, utekaji nyara na mateso, ikiwa ni pamoja na watoto, ikiwa ni pamoja na mauaji ya Wad Al-Noura, Al-Hilaliya, Jalqani, Al-Sariha, Tamboul, kambi ya Zamzam na vijiji vya Kaskazini Darfur, Al-Geneina, Ardumta na vijiji vya jimbo la Nile Nyeupe katikati mwa nchi, ambayo ilisababisha vifo vya maelfu ya raia na kuwahamisha mamia ya maelfu yao. Hii inaongezewa na uhalifu wa unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji wa kimbari dhidi ya wanawake, wasichana na hata watoto.
Mapigano haya yamesababisha watu zaidi ya milioni 14 kuyahama makazi yao, kulingana na Shirika la Uhamiaji la Kimataifa la Umoja wa Mataifa; wakiwemo zaidi ya watu milioni 11 waliokimbia makazi yao ndani ya Sudan, na zaidi ya wakimbizi milioni 3 walikimbilia nchi jirani kama vile Misri, Ethiopia, Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Chad na hata Jordan.
Watoto wanawakilisha 53% ya watu waliokimbia makazi yao ndani ya nchi, na hivyo kuifanya Sudan kuwa mgogoro mkubwa zaidi wa uhamaji wa ndani duniani, ambapo wakimbizi wanachukua takriban theluthi moja ya wakazi wa Sudan wapatao milioni 50. Makambi ya wakimbizi hayana huduma za msingi, na wanakabiliwa na uhaba wa chakula, maji safi na huduma za afya. Pia, makambi haya yanakabiliwa na mashambulizi ya mara kwa mara, ambayo huongeza mateso ya wakimbizi.
Haya yote yamesababisha mgogoro mkubwa wa chakula, hasa kwa kuwa pande zote mbili zinatumia njaa kama silaha ya vita kwa kuzuia chakula kuingia katika maeneo wanayoyadhibiti, ambapo takriban watu milioni 25 - karibu nusu ya idadi ya watu - wanahitaji msaada wa chakula, hasa katika makambi ya wakimbizi. Mamia ya maelfu ya watoto wanakabiliwa na utapiamlo mkali, na idadi kubwa yao iko hatarini kufa. Ripoti zinaonyesha kuwa takriban watoto milioni 3.7 nchini Sudan wanakabiliwa na utapiamlo, huku matarajio ya idadi hii kuongezeka ikiwa hali itaendelea hivi, na uwezekano wa vifo vya takriban watoto 220,000 wanaougua utapiamlo mkali.
Hiyo ni, Sudan, ambayo ilichukuliwa kuwa kikapu cha chakula cha ulimwengu kutokana na wingi wa ardhi ya kilimo, maji na mifugo, sasa watu wake wanakabiliwa na njaa, umaskini, magonjwa na uhamishaji, na inakabiliwa na janga kubwa zaidi la kibinadamu katika nyanja zote kutokana na vita vilivyolaaniwa kati ya jeshi na vikosi vya msaada wa haraka, kuendeleza tu tamaa za bibi yao Marekani nchini Sudan na utajiri wake, ambao unalipiwa gharama kubwa na watu walioathirika wa Sudan pekee.
Mapigano haya yataendelea nchini Sudan na nchi nyingine za Waislamu maadamu tamaa za kikoloni zipo, na watawala wanyonge wamekaa juu ya vifua vyao. Kwa hivyo fanyeni kazi, enyi watu, kuwatoa madarakani na kuanzisha dola ya pili ya Khilafah Rashidah kwa njia ya unabii ili Sudan na nchi zote za Waislamu zikombolewe kutoka katika minyororo ya ukoloni kwa aina na mbinu zake zote. Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hiyo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu si mwenye kubadilisha neema alizowazilia watu mpaka wabadili yaliyomo nafsi zao.﴾
Kama alivyotoa Ibn Majah kwa isnadi yake kwa Abdullah bin Omar, Mwenyezi Mungu awaridhie, akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alitukabili akasema: «Enyi kundi la wahajiri: mambo matano mkiyafanyiwa mtihani, na najikinga kwa Mwenyezi Mungu yasikukuteni; Uovu haujadhihirika katika watu wowote hata wautangaze isipokuwa utawaenea tauni na maradhi ambayo hayajawahi kuwapata waliopita kabla yao, na hawatapunguza kipimo na mizani isipokuwa watachukuliwa kwa miaka na ukali wa gharama na dhuluma ya sultani juu yao, na hawatazuia zaka ya mali yao isipokuwa watazuiwa mvua kutoka mbinguni, na lau si wanyama hawangenyeshewa mvua, na hawatavunja agano la Mwenyezi Mungu na agano la Mtume wake isipokuwa Mwenyezi Mungu atawasaliti adui kutoka kwao, na watachukua baadhi ya yaliyo mikononi mwao, na viongozi wao hawatohukumu kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kuchagua katika aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu atafanya vita vyao baina yao». Na huu ndio hali yetu na hali yetu katika nchi za Kiislamu tangu kuzama kwa jua la Ukhalifa na mchunga na kiongozi anayehukumu kwa sheria ya Mwenyezi Mungu na dini yake.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muslima Al-Shami (Um Suhaib)
Chanzo: Rada