Miongoni mwa Vipengele Vya Kisaikolojia vya Kiislamu
Kipindi cha Tatu
Alhamdulillah Mola Mlezi wa walimwengu, na sala na salamu zimwendee Imamu wa wacha Mungu, na Bwana wa Mitume, aliyetumwa kama rehema kwa walimwengu, Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote, na tujaalie kuwa pamoja nao, na utukusanye katika kundi lao kwa rehema yako, Ee Mrehemu zaidi wa wote wenye kurehemu.
Enyi Waislamu:
Wasikilizaji wapenzi, wasikilizaji wa redio ya afisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir:
Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh, na baada ya hayo: Katika kipindi hichi tunaendelea na tafakuri zetu katika kitabu "Miongoni mwa Vipengele Vya Kisaikolojia vya Kiislamu". Na kwa ajili ya kutoa mifano hai ya tabia ya Kiislamu, huku tukizingatia akili ya Kiislamu, tunasema na kwa taufiki ya Allah: Tulisema katika kipindi kilichopita: "Akili ni jinsi akili inavyoendesha mambo, yaani, kutoa hukumu juu yake kulingana na kanuni ambayo inaamini na kutulia nayo". Hivyo ndivyo Muislamu anapaswa kuwa akisimama kwenye mipaka ya Mwenyezi Mungu, akipima mambo kwa kipimo cha Mwenyezi Mungu, na kuipima kwa mizani ya Mwenyezi Mungu, ambayo ni halali na haramu, akifuata aliyoamrisha Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na kuacha aliyokataza Mwenyezi Mungu na Mtume wake, akifanya hivyo hata kama inapingana na matamanio yake na maslahi yake akitafuta radhi za Mwenyezi Mungu, na hali ya ulimi wake inasema yale aliyosema mshairi:
Laiti unakuwa mtamu ilhali maisha ni machungu Na laiti unaridhika ilhali viumbe wamekasirika
Na laiti yale yaliyo baina yangu na wewe yamejengeka Na baina yangu na walimwengu yameharibika
Ikiwa mapenzi yatakuwa sahihi kutoka kwako, basi kila kitu ni rahisi Na kila kilicho juu ya ardhi ni ardhi
Enyi Waislamu:
Muumini mwenye akili ya Kiislamu «mnyenyekevu, laini, mwerevu, mwangalifu». Kama alivyotueleza mpenzi wetu Mtume Mustafa, sala na salamu za Mwenyezi Mungu zimshukie, kwani muumini anasifika kwa busara na akili, naye ni mwepesi wa kufahamu, kwa maana kwamba katika hali ngumu na za hatari anajitahidi kwa hekima, akijibu jibu la kumnyamazisha adui yake, ambalo linamuokoa na kumwondolea dhiki na aibu, na kumtoa katika mkwamo aliyomweka adui yake, na tutatoa mfano hai wa maisha ya Mtume, swallallahu alayhi wasallam: Katika wasifu wa Ibn Hisham, Ibn Ishaq alisema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, na Abu Bakr, Radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, walipanda mpaka wakasimama juu ya mzee mmoja kutoka kwa Waarabu, wakamuuliza kuhusu Maquraishi na kuhusu Muhammad na masahaba zake na yale aliyoyasikia kuhusu wao, yule mzee akasema: Siwambii mpaka mniambie nyinyi ni akina nani. Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, akasema: «Ukitueleza, tutakueleza» Akasema: Hiyo ni sawa na hiyo? Akasema: «Ndio» Yule mzee akasema: Nimeambiwa kwamba Muhammad na masahaba zake walitoka siku fulani, na ikiwa yule aliyeniambia anasema kweli, wao leo wako mahali fulani kwa mahali ambapo Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alikuwa, na nimeambiwa kwamba Maquraishi walitoka siku fulani, na ikiwa yule aliyeniambia anasema kweli, wao leo wako mahali fulani, kwa mahali ambapo Maquraishi walikuwa, alipomaliza habari zake, akasema: Nyinyi ni akina nani? Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, akasema: «Sisi ni kutoka kwa maji». Kisha akaondoka kwenda zake. Anasema yule mzee: Ni maji gani? Je, ni kutoka kwa maji ya Iraq?
Enyi Waislamu:
Hivi ndivyo inavyopasa kuwa akili ya muumini, akili ya Kiislamu. Anaelewa mambo, yaani, anatoa hukumu juu yake kulingana na kanuni anayoiamini na kutulia nayo. Na anasifika kwa busara na akili, naye ni mwepesi wa kufahamu, anajitahidi kwa hekima, akijibu jibu la kumnyamazisha adui yake, wala si Mtume, swallallahu alayhi wasallam, peke yake ndiye mwenye akili hii ya Kiislamu, bali masahaba, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote, na haswa Khalifa wa kwanza Abu Bakr As-Siddiq, Radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, wana akili kama hii, vipi sivyo ilhali wamelelewa katika shule ya utume?
As-Siddiq, Radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, alifuatana na Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, katika hijra yake kutoka Makka kwenda Madina. Naye anajua kwamba maana ya urafiki huu ni kwamba atakuwa peke yake akifuatana na Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu kwa angalau siku kumi na chache, naye ndiye atakayetoa maisha yake kwa bwana wake na kiongozi wake na mpenzi wake Mtume Mustafa, swallallahu alayhi wasallam, ni ushindi gani katika ulimwengu huu unaozidi ushindi huu? Kwamba As-Siddiq atakuwa peke yake bila ya watu wa ardhini, na bila ya masahaba wote akifuatana na Bwana wa viumbe na urafiki wake kwa muda wote huu? Na maana za mapenzi katika Mwenyezi Mungu zinaonekana katika hofu ya Abu Bakr akiwa ndani ya pango kwamba washirikina watamuona, ili As-Siddiq awe mfano wa kile ambacho askari mwaminifu wa da'wa anapaswa kuwa, pamoja na kiongozi wake mwaminifu, wakati hatari inamzunguka kwa hofu na huruma kwa maisha yake, kwani Abu Bakr wakati huo hakuwa anachelea kifo kwa nafsi yake, na lau angekuwa hivyo hangalifuatana na Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, katika hijra hii hatari, naye anajua kwamba malipo yake madogo ni kuuliwa ikiwa washirikina watamkamata pamoja na Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, lakini alikuwa anaogopa uhai wa Mtume mtukufu, swallallahu alayhi wasallam, na mustakabali wa Uislamu ikiwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, angeangukia mikononi mwa washirikina, na hisia kubwa ya kiusalama ya As-Siddiq inaonekana katika hijra yake na Mtume, swallallahu alayhi wasallam, katika hali nyingi, ikiwemo, alipomjibu yule muulizaji: Huyu ni nani huyu mtu aliye mbele yako? Abu Bakr, Radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie, akasema: Huyu ni muongozaji ananiongoza njia, yule muulizaji akadhani kwamba As-Siddiq anamaanisha njia, lakini alikuwa anamaanisha njia ya kheri, na hili linaashiria matumizi mazuri ya Abu Bakr ya maonyesho, akiepuka aibu au uongo, na linaashiria wazi akili ya Kiislamu anayoifurahia.
Enyi Waislamu:
Je, wanawake wameshindwa kuzaa watu kama hawa wenye akili timamu za Kiislamu? Ili kujibu, tunasema: Hakika mama waliowazaa watu hawa wenye akili timamu za Kiislamu, bado wana uwezo wa kuzaa viongozi wakuu kama hawa ambao sisemi kwa kupita kiasi: Kwamba wao ni kama masahaba, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao! Na tutatoa mfano hai kutoka katika zama zetu tunazoishi, na nilikuwa shahidi wa macho, ninazieleza kwa uaminifu kama nilivyozishuhudia kwa uhalisia: Wakati Mwenyezi Mungu alinishushia heshima ya kuibeba da'wa pamoja na vijana wa Hizb ut-Tahrir, na nilikamatwa mwaka themanini na tatu, na vyombo vya ujasusi katika jimbo la Jordan, na nilikuwa mgeni kwa da'wa, niliwajua vijana wengi wa chama, na nilijifunza kutoka kwao na kutoka kwa msimamo wao wa ujasiri na ushujaa mambo mengi. Na miongoni mwa vijana hawa mashuhuri niliowajifunza kutoka kwao, na nimenufaika nao faida kubwa ni Amir wetu wa sasa, Amir wa Hizb ut-Tahrir Ata bin Khalil Abu Al-Rashtah, Mwenyezi Mungu amuhifadhi na amlinde. Hakika yeye ni mwanamume na mwanamume yeyote! Mtu wa aina yake, mwenye tabia ya Kiislamu ya hali ya juu, mwenye akili ya Kiislamu iliyoangaziwa, na mwenye saikolojia ya Kiislamu miongoni mwa saikolojia bora zaidi. Na huu ni ushahidi wa haki nitakao ulizwa juu yake siku ya Qiyama, ninautoa kwa ajili ya uso wa Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu, na ni ushahidi ninaoutoa na kuuwakilisha kwa umma wa Kiislamu, ili huenda ukaongozwa kwa jambo lake la busara zaidi, na linapogusa njia yake kuelekea kwenye utukufu, na linatafuta kiongozi wa kuliongoza kwenye nchi ya amani! Na analihukumu kwa sheria ya Mola Mlezi wake Rahman! Na anatekeleza ndani yake mwongozo wa Qur'an, na anafanya ndani yake sunna ya Nabii Adnan, swallallahu alayhi wasallam.
Enyi Waislamu:
Nitawakumbusha msimamo mmoja kutoka kwa misimamo mingi ambayo inaonyesha akili ya hali ya juu ya Kiislamu ambayo Amir wetu Amir wa Hizb ut-Tahrir anafurahia, alitoa hotuba akiwa Amman kwa moyo, na alikuwa akiitoa kana kwamba anasoma kutoka kwa kitabu. Na hotuba hii ilikuwa na kichwa: "Mizozo ya Kiuchumi: Uhakika wake na suluhisho lake kutoka kwa mtazamo wa Uislamu" Na baada ya kuimaliza, alitoa fursa ya kuuliza maswali kutoka kwa waliohudhuria. Hata hivyo, vyombo vya ujasusi vilikuwa vimemdunisha mmoja wa washirika wao ili kuharibu hali ya hotuba, hivyo aliharakisha na kuleta swali lifuatalo: Hizb ut-Tahrir ilianzishwa mwanzoni mwa miaka ya hamsini, basi imefanya nini hadi sasa? Basi Abu Yasin alimjibu nini? Fungueni mioyo yenu na akili zenu enyi waumini na sikilizeni, ili kusikia jibu hili linaloonyesha kasi ya kufahamu kwake, Abu Yasin, Mwenyezi Mungu amuhifadhi na amlinde, alisema: "Nimetoa yale niliyokabidhiwa nayo, na asante". Mara tu wahudhuriaji waliposikia jibu hilo, wote waliokuwa ukumbini waliangua kupiga makofi wakivutiwa nalo.
Wasikilizaji wapenzi: Wasikilizaji wa redio ya afisi ya habari ya Hizb ut-Tahrir:
Tunatosheka na kiwango hichi katika kipindi hichi, ili tukamilishe tafakuri zetu katika vipindi vijavyo InshaAllah Ta'ala, mpaka wakati huo na mpaka tutakapokutana nanyi, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu na hifadhi yake na amani yake. Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.