Mfululizo wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu"
Na Mwandishi na Mwanafikra Thair Salama – Abu Malik
Sehemu ya Thelathini na Nane: Umuhimu wa Allah kuwateua Waislamu na nguvu ya Ukhalifa kuwa sababu kuu ya kuhifadhi Dini1 - Sehemu ya 2
Hizi ndizo tafsiri, na tuanze na Ijma, kisha Tawatur ya maana:
Ijma katika lugha: Azma ya jambo na kulikusudia, au makubaliano.
Ama Ijma katika istilahi ya Wanazuoni wa Usuli ni makubaliano juu ya hukumu ya tukio miongoni mwa matukio kwamba ni hukumu ya kisheria, katika zama zisizo za Mtume ﷺ, kwa hiyo Ijma inachukua nafasi ya dalili ya kisheria (kutoka katika Sunna)2 na Ijma baada ya zama za Masahaba: ni makubaliano ya Mujtahidina katika zama za Tabiina au wafuasi wao na kadhalika, kutoka katika umma wa Muhammad ﷺ juu ya jambo miongoni mwa mambo,
Na ni lazima kupambanua kati ya Ijma, na kati ya hukumu ya kisheria ambayo inapatikana kwa ijtihadi, kwa sababu katika akili za wanazuoni wengi leo, na vile vile hapo awali, kuna wazo la ijtihadi ya pamoja, ambapo wingi wa maoni unatoa nguvu kwa ijtihadi, kwa hivyo wanafikiria Ijma kwa namna hii, kama vile ijtihadi ya umati mkubwa, au kukubaliana kwa Mujtahidina katika zama juu ya hukumu fulani ya kisheria, kwa hivyo ni hukumu ya kisheria ambayo inatambulika kwa nguvu ya wingi wa walioitoa, kwa hivyo kwa taswira hii wanaiondoa Ijma kutoka katika sifa ya dalili, hadi sifa ya hukumu ya kisheria! Kwa hiyo Ijma inakuwa chombo cha kupendelea ijtihadi tu kwa sababu ya wingi wa walioafikiana na rai hiyo!
Na taswira hii siyo maana ya Ijma, kwa hiyo Ijma ni kunukuu hukumu, au kwa namna sahihi zaidi: makubaliano juu ya hukumu ya tukio miongoni mwa matukio kwamba ni hukumu ya kisheria, kwa hiyo uhujaji wake katika matokeo unamaanisha kusimamisha makubaliano yanayopatikana katika zama zozote juu ya jambo, au jambo la kidini au hukumu ya taklifu kuwa dalili ya kisheria juu ya hukumu! Kwa hiyo kile walichoafikiana Masahaba, au kile walichoafikiana wanazuoni wa umma- kwa anayesema kwa namna hii ya Ijma- inasimama kama dalili juu ya hukumu! Kisha inatolewa kutoka kwake, kama inavyotolewa kutoka katika Qur'an au Sunna, kwa hiyo inafichua kuwepo kwa dalili, kwa hiyo Ijma ni dalili miongoni mwa dalili ambazo zinatolewa kutoka kwake, kwa hiyo hili ndilo linaloitofautisha na hukumu ya kisheria ambayo tumeifikia kwa ijtihadi!
Kumbuka ewe aliyelindwa na Allah kwamba hukumu ni ya Allah pekee, na wala haichukuliwi hukumu ila kutoka katika wahyi, na wala haisimami onyo ila kwa wahyi, na wala haisifiki uzito wa chembe ya amali kwa kheri na shari na inafaa kuhesabiwa juu yake ila ikiwa imetegemea wahyi, na wala haisimami hoja juu ya watu ila kwa yale yaliyoteremshwa katika wahyi, na wala hakuacha watu bure, na haya yote yanaashiria kwamba sisi hatutarajii kutoka kwa wanadamu kukubaliana juu ya jambo "lililosahauliwa na sheria" au "wamesahau", na kwa msingi huo Ijma lazima ifikishe rai kwa wahyi ili iwe ni yenye msingi, na wahyi umekatika baada ya Mtume ﷺ, kwa hiyo inabaki maana ya Ijma tu: kufichua dalili, au kunukuu dalili kutoka katika Sunna!
Na labda matatizo muhimu yanayohusiana na Ijma ni:
-
Nini Ijma inayokubalika? (Ijma ya Masahaba, Ijma ya umma, Ijma ya kizazi cha Mtume, Ijma ya Mujtahidina wa zama...)
-
Ijma inafungamana na nani? na namna ya kuzingatia maoni ya anayekhalifu.
-
Je, hukumu inayotokana na Ijma ni bayana au kunukuu dalili juu ya hukumu ya kisheria iliyoambatana na wahyi au ni kuunda hukumu mpya ambayo chanzo chake ni maoni na akili za walioafikiana?
1- Mwalimu Mwanafikra Youssef Al-Sarisi.
2- Angalia Taysir Al-Wusul Ila Al-Usul cha Alama Ata Abu Al-Rashta, sehemu ya kwanza ukurasa wa 82. Na kama tulivyotangulia kusema Masahaba walinukuu Qur'an na Sunna, kwa hiyo Qur'an Tukufu hakuna shaka kwamba ilinukuliwa kikamilifu, kwa hivyo mada ya ijtihadi ya kutoa hukumu kutoka kwake inapatikana katika maandishi yake, anaweza kuifanya Mujtahid yeyote katika zama zozote, hakuna ndani yake kilichofichika, na Sunna walitunukulia kwa kauli na vitendo na kukubali, na baadhi ya Sunna hizi zimewakilishwa katika masuala ambayo yamekuwa miongoni mwa mambo ya msingi katika jamii ambapo hakuna haja ya kusema Mtume wa Allah ﷺ alisema kadha wa kadha, kwa hiyo ilinukuliwa kwa sura ya Ijma ambayo ilitufichulia kuwepo kwa dalili kutoka katika Sunna ambayo Masahaba walitegemea wakati wa Ijma yao!