Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Kwa Mwandishi na Mwanafikra Thaer Salama - Abu Malik - Sehemu ya 48
Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Kwa Mwandishi na Mwanafikra Thaer Salama - Abu Malik - Sehemu ya 48

Ukhalifa ni kusimama kitu mahali pa kitu, na hukumu ni ya Mwenyezi Mungu, na amewajaalia viumbe kwa ujumla kwa kauli yake ﷺ: «Hakika dunia ni tamu na ya kijani kibichi, na Mwenyezi Mungu anakufanyeni makhalifa ndani yake, ili aone mnavyotenda» Imepokewa na Muslim kutoka kwa Abu Saeed Al-Khudri, kuthibitisha kauli yake Mwenyezi Mungu ﴿Kisha tukakufanyeni makhalifa katika ardhi baada yao ili tuone mnavyotenda﴾ [Yunus: 14], yaani mtekeleze hukumu za Mwenyezi Mungu, na manhaj ya Mwenyezi Mungu baina yenu na juu ya nafsi zenu katika kila jambo, na ukhalifa kwa khasa katika hukumu, kutoka kwa mtawala anahukumu kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu, kwani manhaj hii ndio inayotofautisha baina ya anayefanywa khalifa katika ardhi awe ni mharibifu ndani yake, mtoaji damu, au awe ni khalifa anaye kingwa na manhaj hiyo kutokana na kosa hilo, na ili itawale manhaj lazima itawale kupitia dola, siyo tu kwamba wafuate watu katika jamii ambayo inatawaliwa na manhaj isiyo hiyo!

0:00 0:00
Speed:
August 16, 2025

Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Kwa Mwandishi na Mwanafikra Thaer Salama - Abu Malik - Sehemu ya 48

Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu"

Kwa Mwandishi na Mwanafikra Thaer Salama – Abu Malik

Sehemu ya Arobaini na Nane: Falsafa ya Uislamu kuhusu Ukhalifa – J1

Ukhalifa ni kusimama kitu mahali pa kitu, na hukumu ni ya Mwenyezi Mungu, na amewajaalia viumbe kwa ujumla kwa kauli yake ﷺ: «Hakika dunia ni tamu na ya kijani kibichi, na Mwenyezi Mungu anakufanyeni makhalifa ndani yake, ili aone mnavyotenda» Imepokewa na Muslim kutoka kwa Abu Saeed Al-Khudri, kuthibitisha kauli yake Mwenyezi Mungu ﴿Kisha tukakufanyeni makhalifa katika ardhi baada yao ili tuone mnavyotenda﴾ [Yunus: 14]1, yaani mtekeleze hukumu za Mwenyezi Mungu, na manhaj ya Mwenyezi Mungu baina yenu na juu ya nafsi zenu katika kila jambo, na ukhalifa kwa khasa katika hukumu, kutoka kwa mtawala anahukumu kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu, kwani manhaj hii ndio inayotofautisha baina ya anayefanywa khalifa katika ardhi awe ni mharibifu ndani yake, mtoaji damu, au awe ni khalifa anaye kingwa na manhaj hiyo kutokana na kosa hilo, na ili itawale manhaj lazima itawale kupitia dola, siyo tu kwamba wafuate watu katika jamii ambayo inatawaliwa na manhaj isiyo hiyo!

Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿Hakika Mimi nitaweka katika ardhi khalifa﴾ Alisema Al-Qurtubi Mwenyezi Mungu amrehemu: Aya hii ni asili katika kuteua imamu na khalifa anasikilizwa na kutiiwa; ili kusanyika neno naye, na zitekelezwe kwake hukumu za khalifa. Na hakuna khilafu katika wajibu wa hilo baina ya umma wala baina ya maimamu ila aliyo simuliwa kutoka kwa Al-Asam kwani alikuwa kuhusu sheria ni kiziwi, mwisho, na hili ni katika usahihi wa elimu ya Imamu Al-Qurtubi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake!

Na hiyo ni kuwa Mwenyezi Mungu ameisimamisha mbingu na ardhi juu ya uadilifu, kama ilivyo katika hadithi Qudsiy kutoka kwa Abu Dhar Jundub bin Junada, Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Nabii ﷺ katika anayo simulia kutoka kwa Mwenyezi Mungu Tabaraka wa Ta'ala ﷻ, Mola wa Ukuu, zimetakasika majina yake kwamba amesema: «Enyi waja wangu mimi nimeharamisha dhulma juu ya nafsi yangu na nimeifanya baina yenu ni haramu basi msidhulumiane», basi Mwenyezi Mungu ameharamisha dhulma juu ya nafsi yake, na ameiharamisha juu ya waja na akateremsha sheria, na manhaj ambayo inahakikisha kwamba hauingii uonevu katika ufalme wa mbingu na ardhi, akamfanya mwanadamu kuwa khalifa ili asimamishe mfumo ambao unasimamisha uadilifu, na unazuia uonevu, ﴿Hakika tuliwatuma Mitume wetu kwa hoja zilizo wazi, na tukateremsha pamoja nao Kitabu na Mizani, ili watu wasimame kwa uadilifu﴾ [Al-Hadid: 25], akajaalia mamlaka kwa umma inamuwakilisha hakimu anayewahukumu kwa sheria ya Mola wake, kama ilivyo thibiti kutokana na kuchimbua kutoka katika asili za mfumo wa utawala katika Uislamu, basi khalifa aliyetajwa ni waumini wanaofuata sheria ya Mwenyezi Mungu katika aliyo waamrisha kuyasimamisha katika maisha yao, wanaosimamisha manhaj yake ndani yao, kama tulivyo tanguliza, kwani kusimama manhaj katika watu binafsi hakuiamishi katika jamii, na isiposimama katika jamii haitatimia kuhukumu kwao kwake2, na wala hautatimia uadilifu, kwa hivyo imepelekea jambo kusimama manhaj katika watu binafsi na jamii na dola, na kwani hukumu nyingi kati ya hizi zinatumiwa kupitia dola, basi watu humpa bai'a juu yake khalifa anazisimamisha ndani yao, basi lilikuwa kujaaliwa khalifa hakimu pia ni maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ﴿Na pale Mola wako alipo waambia Malaika: Mimi nitaweka katika ardhi khalifa﴾, yaani ambaye kwake inatimia maana ya kutafutwa ukhalifa utimia unaopelekea makusudio kutokana na utafutaji huo, katika anayodokeza aya kama alivyochimbua Al-Qurtubi, kwa hivyo waliuliza Malaika Mola wa Ukuu Subhanahu wa Ta'ala: ﴿Wakasema: Utamuweka humo atakaye fanya ufisadi na kumwaga damu?﴾ khalifa? Akasema haki Ta'ala akijibu: ﴿Akasema: Hakika Mimi najua msiyo yajua﴾, na wala si katika maana kuwa khalifa ni sitiari kuhusu mwanadamu anafanya analo taka, lau ingelikuwa hivyo, ingelitimia maana ya kukataa kwao: ﴿Wakasema: Utamuweka humo atakaye fanya ufisadi na kumwaga damu?﴾, ama kwani amewajibu Mola wa Ukuu akisema: ﴿Hakika Mimi najua msiyo yajua﴾ basi ndani yake mna maana kwamba hakumfanya khalifa kwa ajili ya kumwaga damu, na kufanya ufisadi, na kutokana na hili tunawatoa katika utafutwaji anayefuata manhaj yoyote inapelekea kufanya ufisadi na kumwaga damu, na huu ni hali ya kila manhaj iliyosimama juu ya kutunga sheria watu, na matamanio yao, kuthibitisha kauli yake Mwenyezi Mungu: ﴿Na lau Haki ingelifuata matamanio yao, zingelifisidika mbingu na ardhi na vilivyomo﴾ [Al-Mu'minun: 71], ﴿Kisha tukakuweka juu ya sheria katika jambo basi ifuate wala usifuate matamanio ya wasiojua﴾ [Al-Jathiya: 18], basi isiyo sheria ya Mwenyezi Mungu ni kufuata matamanio ya watungao sheria, na inapelekea kufanya ufisadi katika ardhi, kwa hivyo khalifa anayeashiriwa ni ambaye anasimamisha manhaj ya Mwenyezi Mungu ambayo inahakikisha kuthibitisha haki na uadilifu kulingana na sheria ya Mwenyezi Mungu, kwa kutumia sheria yake huyu ndiye aliyemtafuta Mwenyezi Mungu Ta'ala: Waumini wanasimamisha sheria yake na wanamupa bai'a khalifa anaitumia ndani yao.

Na akasema Mola wa walimwengu Subhanahu wa Ta'ala: ﴿Ewe Daudi! Hakika tumekufanya khalifa katika ardhi, basi hukumu baina ya watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza njia ya Mwenyezi Mungu﴾ [Sad: 26], na hiyo inalingana na kuwa Mwenyezi Mungu ameteremsha vitabu vhukumu baina ya watu kwa haki, ﴿Watu walikuwa umma mmoja, kisha Mwenyezi Mungu akawapeleka Manabii, watoao bishara na waonyaji. Na akateremsha pamoja nao Kitabu kwa Haki ili kihukumu baina ya watu katika yale waliyo khitalifiana﴾ basi kumtafuta Daudi Amani iwe juu yake na kuhukumu kwake baina ya watu kwa haki ni kama kumtafuta Muhammad ﷺ na kuhukumu kwake baina ya watu kwa haki ﴿Na uhukumu baina yao kwa aliyo teremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao, na tahadhari nao wasije kukufitini ukaacha baadhi ya aliyo kuteremshia Mwenyezi Mungu﴾ [Al-Maidah: 49], na hii ndani yake mna khitabu kwa Mtume ﷺ na ni khitabu kwa umma wake, basi kutafuta ilikuwa kusimama kwa hukumu za Mwenyezi Mungu katika waja, na ndio asili katika kila sheria ya kimungu, na kila kitabu kilicho teremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu kimeteremshwa ili kihukumu, na walikuwa wana wa Israel wanatawaliwa na Manabii kwa vitabu hivyo na sheria za kimungu, kisha ikahamia sunna hii kwa Makhalifa baada ya Mtume ﷺ kama ilivyo katika hadithi ya Bukhari kutoka kwa Abu Hazim alisema: Nilikaa na Abu Huraira miaka mitano nikamsikia anasimulia kutoka kwa Nabii ﷺ alisema: «Walikuwa wana wa Israel wanatawaliwa na Manabii kila alipoangamia Nabii alifuatwa na Nabii, na hakika hakuna Nabii baada yangu na watakuwa Makhalifa watakuwa wengi, walisema unatatuamrisha nini? Alisema: timizeni bai'a ya wa kwanza kisha wa kwanza na wapeeni haki yao, kwani Mwenyezi Mungu atawauliza kuhusu walicho pewa kukichunga» [Imepokewa na Muslim na Bukhari na Ibn Hanbal na Ibn Majah], basi ametaja kwamba siasa ya umma itakuwa kwa Nabii ﷺ kisha kwa Makhalifa baada yake, na akaamrisha kuwatii na kutimiza bai'a yao, na kutoka kwa Abu Saeed Al-Khudri kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ kwamba alisema: «Akipewa bai'a Makhalifa wawili basi muuweni yule mwingine kati yao», akaamrisha umoja wa dola ya Ukhalifa na akamfanya anayetenganisha jamaa ya Waislamu ni halali ya damu, amesimulia Muslim katika kitabu cha Uimara: «Kutoka kwa Arfaja alisema nimemsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ anasema anayekujieni na amri yenu ni jamaa juu ya mtu mmoja anataka kuigawanya fimbo yenu au kuifarikisha jamaa yenu basi muueni».

1- Na kauli yake Mwenyezi Mungu Ta'ala: ﴿Naye ndiye aliyekufanyeni makhalifa katika ardhi, na akawainua baadhi yenu juu ya wengine kwa daraja, ili akujaribuni katika aliyo kupeni. Hakika Mola wako ni Mwepesi wa kuadhibu, na hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu﴾ 165 Al-An'am, na kauli yake Mwenyezi Mungu Ta'ala: ﴿Yeye ndiye aliyekufanyeni makhalifa katika ardhi﴾ 39 Fatir.

2- Jiwe la msingi katika utambulisho wa jamii ni namna ambayo zinaendeshwa kwayo mahusiano, na kanuni ambazo zinadhibiti mahusiano haya, basi mahusiano ya riba ni matokeo ya kutumia mfumo wa kirasilimali  mathalan, haiwezekani kubadilika katika jamii maadamu imebakia jamii ni ya kirasilimali, na wala hakuna athari ya kukataa mamilioni ya watu miongoni mwa Waislamu katika jamii za kimagharibi au hata nchi za Kiislamu ambazo unatawanyika ndani yake mfumo wa riba kuhusu riba katika kubadilisha mfumo wa kiuchumi wa kirasilimali ndani yake, bali wao bila shaka zitaingia pesa zao benki, na zitazitumia benki kwa namna ya kisheria katika anayoyaona benki, na zichanganyike pesa za Waislamu na riba na na biashara ya pombe, na vitega uchumi ambavyo zinavitega benki katika vilabu vya usiku, wametaka Waislamu katika magharibi au wamekataa, bali na juu ya hivyo, basi watakubali sheria za dola kutokana na bima ya lazima, na kanuni zilizoharamishwa katika Uislamu na mengineyo, basi muhula kwa hivyo katika mahusiano na kanuni siyo katika itikadi za watu binafsi.

More from Mawazo

Tafakari katika kitabu: "Miongoni mwa nguzo za Saikolojia ya Kiislamu" - Kipindi cha kumi na saba

Tafakari katika kitabu: "Miongoni mwa nguzo za Saikolojia ya Kiislamu"

Imeandaliwa na Ustadh Muhammad Ahmad Al-Nadi

Kipindi cha kumi na saba

AlhamduliLlah, Mola Mlezi wa walimwengu, na rehema na amani zimshukie imamu wa wachaMungu, na bwana wa Mitume, aliyetumwa kama rehema kwa walimwengu, Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote, na tujaalie kuwa pamoja nao, na utuhusishe katika kundi lao kwa rehema yako, Ee Mwingi wa rehema kuliko wote wenye kurehemu.

Wasikilizaji wangu wapenzi, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:

Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh, na baada ya hayo: Katika kipindi hiki tunaendelea na tafakari zetu katika kitabu: "Miongoni mwa nguzo za Saikolojia ya Kiislamu". Na kwa ajili ya kujenga haiba ya Kiislamu, pamoja na kuzingatia akili ya Kiislamu na saikolojia ya Kiislamu, tunasema na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu:

Ama chuki kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu Subhanahu amekataza kuwapenda makafiri, wanafiki, na waovu wanaoonekana waziwazi, kwa kauli yake Taala: {Enyi mlio amini! Msiwafanye maadui zangu na maadui zenu kuwa marafiki, mkiwapelekea mapenzi, na hali wao wamekwisha kataa haki iliyo kufikieni, wanamfukuza Mtume na nyinyi kwa sababu ya kumwamini Mwenyezi Mungu, Mola wenu Mlezi, ikiwa mmetoka kupigana jihadi katika njia yangu na kutafuta radhi yangu. Mnawaficha mapenzi, na Mimi ninajua mnaficha na mnadhihirisha. Na anaye fanya hivyo miongoni mwenu basi amekwisha potea njia iliyo sawa}. (Al-Mumtahina 1)

Na kauli yake Taala: {Enyi mlio amini! Msiwafanye watu wa nje kuwa siri zenu. Hawataacha kukuharibuni, wanapenda mtaabike. Uadui umekwisha dhihirika katika vinywa vyao, na yale wanayo yaficha vifuwani mwao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni ishara, ikiwa mnazingatia. Hivyo ndivyo nyinyi! Mnawapenda, lakini wao hawakupendeni, na nyinyi mnaamini Kitabu chote. Wanapo kuoneni husema: Tumeamini. Na wanapo kuwa peke yao, huuma ncha za vidole kwa hasira juu yenu. Sema: Kufeni kwa hasira zenu hizo. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani}. (Al-Imran 119)

Na Al-Tabarani amepokea kwa isnadi nzuri kutoka kwa Ali Karramallahu Wajhahu katika Pepo, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "Mambo matatu ni haki: Mwenyezi Mungu hamfanyi yule ambaye ana sehemu katika Uislamu kama yule ambaye hana sehemu, na Mwenyezi Mungu hamtawalishi mja kisha akamtawalisha mwingine, na mtu hampendi watu isipokuwa atafufushwa pamoja nao." Na katika hili kuna katazo la wazi la kuwapenda watu wabaya kwa hofu ya kufufushwa pamoja nao.

Na Al-Tirmidhiy ametoa katika Sunan yake, na akasema hii ni hadithi nzuri, kutoka kwa Sahl bin Muadh bin Anas Al-Juhani, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, kwamba alisema: "Yeyote anayetoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na anazuia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na anapenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na anamchukia kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na anaoa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, basi amekamilisha imani yake." Na vivyo hivyo Muslim amepokea kutoka kwa Abu Hurairah, ambaye alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "Hakika Mwenyezi Mungu anapompenda mja humwita Jibril na kusema: Mimi nampenda fulani, basi mpende. Akasema: Jibril humpenda, kisha hutangaza mbinguni na kusema: Hakika Mwenyezi Mungu anampenda fulani, basi mpendeni. Watu wa mbinguni humpenda, akasema: Kisha huwekwa kwake kukubalika duniani. Na anapomchukia mja humwita Jibril na kusema: Mimi namchukia fulani, basi mchukie. Akasema: Jibril humchukia, kisha hutangaza kwa watu wa mbinguni kwamba Mwenyezi Mungu anamchukia fulani, basi mchukieni, akasema: Humpa.

Na kauli yake, swallallahu alayhi wasallam: "Kisha huwekwa kwake chuki duniani" ni habari ambayo inakusudiwa kuombwa, na hiyo ni kwa dalili ya mahitaji, kwani kuna makafiri wengi, wanafiki, na waovu wanaoonekana waziwazi, kuna watu wanaowapenda na hawa wachukii, kwa hivyo ukweli wa mtoaji habari unahitaji kwamba kusudi la habari hiyo liwe uanzishaji, ambayo ni ombi, kana kwamba anasema: Enyi watu wa dunia, wachukieni wale ambao Mwenyezi Mungu amewachukia.

Kwa hivyo, hadithi inaonyesha ulazima wa kumchukia yule ambaye Mwenyezi Mungu amemchukia, na chini yake ni ulazima wa kumchukia mpinzani mkali, aliyetajwa katika hadithi ya Aisha iliyokubaliwa na wote kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "Hakika mtu anayechukiwa zaidi na Mwenyezi Mungu ni mpinzani mkali", na ulazima wa kumchukia yule anayewachukia Ansar aliyetajwa katika hadithi ya Al-Bara iliyokubaliwa na wote, alisema: Nilisikia Mtume, swallallahu alayhi wasallam: au alisema: Mtume, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "Ansar hawawapendi isipokuwa muumini, na hawawachukii isipokuwa mnafiki, basi yeyote anayewapenda, Mwenyezi Mungu humpenda, na yeyote anayewachukia, Mwenyezi Mungu humchukia." Na ulazima wa kumchukia yule anayesema ukweli kwa ulimi wake na hauvuki koo lake, kwa hadithi iliyotolewa na Muslim kutoka kwa Busr bin Saeed kutoka kwa Ubaidullah bin Abi Rafi, mtumwa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, kwamba Al-Haruriyyah walipotoka akiwa na Ali bin Abi Talib, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, walisema: Hakuna hukumu ila ya Mwenyezi Mungu. Ali alisema: Neno la haki ambalo linakusudiwa kwa batili, hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, aliwasifu watu, najua sifa zao katika hawa "wanasema ukweli kwa ndimi zao, hii haipiti kutoka kwao - na alielekeza kwenye koo lake - miongoni mwa viumbe wanaochukiwa zaidi na Mwenyezi Mungu kwake." Kauli yake "haipiti" inamaanisha haizidi, na ulazima wa kumchukia mchafu na mwenye matusi aliyetajwa katika hadithi ya Abu Al-Dardaa kwa Al-Tirmidhiy, na akasema hii ni hadithi nzuri sahihi kwamba Mtume, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "... Na hakika Mwenyezi Mungu anamchukia mchafu na mwenye matusi."

Haya, baadhi ya athari zimepokelewa kuhusu chuki ya Masahaba kwa makafiri, mojawapo ikiwa ni yale aliyoyasimulia Muslim kutoka kwa Salama bin Al-Akwaa, alisema: "... Tuliposuluhishwa sisi na watu wa Makka, na baadhi yetu tulichanganyika na wengine, nilikuja kwenye mti, nikaondoa miiba yake, nikazamia chini yake, akasema: Walinijia watu wanne kutoka kwa washirikina, kutoka kwa watu wa Makka, wakaanza kumtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, nikawachukia, nikaenda kwenye mti mwingine..."

Na miongoni mwao ni hadithi ya Jabir bin Abdullah kwa Ahmad kwamba Abdullah bin Rawaha aliwaambia Mayahudi wa Khaibar: "Enyi kundi la Mayahudi, nyinyi ni viumbe vinavyochukiwa zaidi kwangu, mliwaua manabii wa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na Mtukufu, na mlimdanganya Mwenyezi Mungu, na chuki yangu kwenu haitanifanya niwe katili kwenu..."

Na miongoni mwao ni yale yaliyopokelewa kuhusu chuki ya yule anayeonyesha uovu kutoka kwa Waislamu, Ahmad, Abd Al-Razzaq na Abu Ya'la wametoa kwa isnadi nzuri, na Al-Hakim katika Al-Mustadrak, na akasema ni sahihi kwa sharti la Muslim kutoka kwa Abu Firas, alisema: Omar bin Al-Khattab alihutubia, akasema: "... Na yeyote kati yenu anayeonyesha uovu, tutamfikiria uovu, na tutamchukia kwa hilo."

Upendo kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na chuki kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ni miongoni mwa mambo makuu ambayo Muislamu anayeutafuta radhi za Mwenyezi Mungu, rehema, ushindi na pepo yake anasifika nayo.

Wasikilizaji wangu wapenzi: Wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:

Tunatosheka na kiwango hiki katika kipindi hiki, ili tukamilishe tafakari zetu katika vipindi vijavyo, InshaAllah Taala, mpaka wakati huo na mpaka tukutane nanyi, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, hifadhi na usalama wake. Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri na Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh.

Jueni Enyi Waislamu! - Kipindi cha Kumi na Saba

Jueni Enyi Waislamu!

Kipindi cha Kumi na Saba

Kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم alikuwa akiwachagua watawala wake kutoka kwa watu wema kwa ajili ya hukumu na watu wa elimu wanaojulikana kwa uchaji Mungu, na aliwachagua kutoka kwa wale ambao wanajua vizuri kazi katika kile wanachokikabidhiwa, na kuingiza katika mioyo ya raia imani na heshima kwa dola, kutoka kwa Suleiman bin Buraidah kutoka kwa baba yake alisema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم alikuwa akimteua amiri juu ya jeshi au kikosi, alimusia kwa nafsi yake kumcha Mwenyezi Mungu na wote waliokuwa pamoja naye miongoni mwa Waislamu kheri," amesimulia Muslim, na mtawala ni amiri juu ya utawala wake, hivyo anaingia chini ya hadithi hii.