Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Mwandishi na Mwanafikra Thair Salama - Abu Malik - Sehemu ya 4
Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Mwandishi na Mwanafikra Thair Salama - Abu Malik - Sehemu ya 4

Na wanachuoni wamebainisha makusudio manane muhimu kwa mwanadamu nayo ni: kuhifadhi nafsi, mali, dini, akili, kizazi, kuhifadhi dola, kuhifadhi usalama na kuhifadhi heshima ya kibinadamu, na tunaweza kuongeza kwake makusudio makuu yaliyobainishwa kutoka katika aya hizi: kusimamisha uadilifu, kutekeleza sheria, huruma, ibada, uongofu na kubainisha hukumu.

0:00 0:00
Speed:
July 03, 2025

Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu" - Mwandishi na Mwanafikra Thair Salama - Abu Malik - Sehemu ya 4

Msururu wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu"

Mwandishi na Mwanafikra Thair Salama – Abu Malik

Sehemu ya Nne: Kusimamisha Ukhalifa ni miongoni mwa Makusudio Makuu ya Sharia Sehemu ya 2

Na wanachuoni wamebainisha makusudio manane1 muhimu kwa mwanadamu nayo ni: kuhifadhi nafsi, mali, dini, akili, kizazi, kuhifadhi dola, kuhifadhi usalama na kuhifadhi heshima ya kibinadamu, na tunaweza kuongeza kwake makusudio makuu yaliyobainishwa kutoka katika aya hizi: kusimamisha uadilifu, kutekeleza sheria, huruma, ibada, uongofu na kubainisha hukumu.

Basi dini kwa hakika: imeteremshwa ili iwe mfumo wa maisha ambao unawahukumu watu kwa hukumu zake katika maisha yao kwa wajibu2, ﴿WANADAMU WALIKUWA UMMAT MMOJA, ALLAH AKAWAPELEKEA NABII KUWA WA BASHIRI NA WA ONYO NA AKATEREMSHA PAMOJA NAO KITABU KWA HAKI ILI HUKUMU KATI YA WATU KATIKA YALE WANAYOTOFATIANA﴾ [Al-Baqara: 213], na lamu katika kauli yake ﴿ILI HUKUMU KATI YA WATU﴾ ni lamu ya sababu, basi moja ya makusudio muhimu ya ujumla ya kupelekwa Manabii na pamoja nao bishara na onyo ni kwamba Kitabu kihukumu baina ya watu ili kuboresha maisha yao na haki na uadilifu vitawale katika kila jambo la mambo yao ya maisha!, na kwa hiyo basi kutekelezwa kwa hukumu hizi katika uhalisia wa maisha hakika ni makusudio makuu ya sharia, na makusudio ya kutumwa Mtume ﷺ, na makusudio ya kuteremshwa Kitabu! na msingi wa dini imara, na kusimamisha kwake katika maisha ya watu hakika ni miongoni mwa wajibu ulio muhimu zaidi, basi kusimamisha dola ya Kiislamu, yaani dola ya Ukhalifa ni njia ambayo kupitia kwake yanatimizwa makusudio ambayo kwa ajili yake Allah amemtumwa Mtume ﷺ, na ambayo kwa ajili yake ameteremsha Kitabu!

Na vinginevyo basi Uislamu si falsafa ya kufikirika, bali umeteremshwa ili utekelezwe na uhukumu, na imethibitishwa kwamba hukumu hizi hakika zinasimamishwa katika maisha ya Waislamu kupitia dola inayoongoza3, inayoendeshwa na mfumo wa hukumu uliopangwa kisheria ambao Mtume ‏ﷺ ameiita dola ya Ukhalifa4, na akaisimamisha kivitendo, na akasimamisha taasisi zake, na sheria zake, ikapatikana dola kweli, na haikuwa miongoni mwa jambo la Masahaba kuelekea kwake ila kuendeleza yale aliyoanza Bwana wa viumbe ‏ﷺ kuhusu hilo, basi ni dola ambayo nguzo zake zimeegemea kwenye kitendo cha Mtume ‏ﷺ, na kwenye hukumu ambazo zinawakilisha wingi wa Qur'an na Sunnah ambazo ziliteremshwa ili zitekelezwe kupitia kwake, ambazo Masahaba wamekubaliana juu ya ulazima wake kwa ijmai yao, na ulazima wake umeenea kwa njia ya maana, na hawezi kulijua jambo kama hilo la dola kuwepo na hukumu na taasisi, au kusema kuwa ni mfumo wa kibinadamu usio lazima ila mjinga!

 1- Imamu Shatibi amebainisha makusudio matano muhimu: nayo ni kuhifadhi nafsi, mali, dini, akili na kizazi, na ameongeza kwake Imamu Taqiuddin Nabhani makusudio ya kuhifadhi usalama, na makusudio ya kuhifadhi dola, na makusudio ya kuhifadhi heshima ya kibinadamu, kwa kuyabainisha kupitia ukali wa adhabu kwa mtendaji wa uhalifu unaoyagusa kisheria, basi anayetoka nje ya dola kwa silaha anapigwa vita, na anayepasua fimbo ya utiifu na kuapa bay'a kwa Khalifa wa pili anauawa, na mengineyo katika hukumu na maelezo marefu marejeo yake ni kitabu cha haiba ya Kiislamu juzuu ya tatu, yakawa makusudio muhimu ni manane.

2- Hakika faradhi ya Swala, na faradhi ya Zaka ni miongoni mwa faradhi kubwa za Uislamu, lakini faradhi bila ya kutekelezwa, inasababisha adhabu kali, kwa sababu faradhi na hukumu zingine hakika zimeteremshwa ili zitekelezwe na kufanyiwa kazi, basi Uislamu si falsafa ya kufikirika, wala jamhuri zilizo bora, bali ni hukumu zilizoteremshwa kwa ajili ya utekelezaji, na hakika imesimama dola katika Uislamu, na imefaradhishwa Ukhalifa na Muumbaji, kwa sababu kupitia kwake kuna utekelezaji wa faradhi zote na wajibu na hukumu, bali zaidi ya 90% ya hukumu za Uislamu! Na Abu Bakr radhi za Allah ziwe juu yake alilifahamu hilo kwa ufahamu wa kweli kwani alisema: Wallahi nitawapiga vita wanaotenganisha baina ya Swala na Zaka, kwani Zaka ni haki ya mali, Wallahi lau wangenizuia kamba ya ngamia walikuwa wakimlipa Mtume wa Allah ningewapiga vita kwa kuzuia kwake. Basi alipigana kwa sifa yake ya kuwa Khalifa wa Waislamu na aliyemzuia Zaka, basi Zaka inatolewa kwake yeye yaani kwa Sultan!

3- Rejea kitabu chetu: Je, Mtume ﷺ alibainisha njia ya kusimamisha dola ya Kiislamu, basi ndani yake kuna maelezo marefu na dalili imara kwamba Mtume ﷺ alikuwa akifanya kazi ya kuleta dola, na anasema Ibn Taymiyyah katika kitabu cha Siasa ya Kisharia uk. 114 na Majmu'u al-Fatawa j 28/ uk 390: Inawajibika kujua kwamba watawala wa mambo ya watu ni miongoni mwa wajibu mkubwa wa dini bali hakuna usimamaji wa dini ila kwao kwani wanadamu hawakamilishi maslahi yao ila kwa kukutana kwa haja ya baadhi yao kwa wengine na ni lazima kwao wakati wa kukutana kuwa na haja ya kichwa. Na alisema Dkt. Dhiyauddin al-Rais katika kitabu chake Uislamu na Ukhalifa uk 99: "Basi Ukhalifa ni wadhifa muhimu wa kidini na unaowahusu Waislamu wote, na hakika sharia ya Kiislamu imeeleza kwamba kusimamisha Ukhalifa ni faradhi ya msingi miongoni mwa faradhi za dini bali ni faradhi iliyo kuu zaidi kwa sababu utekelezaji wa faradhi zingine unategemea kwake" Angalia: Tanbihi ya wenye kusahaulika na uelezaji kwa wenye kuchanganyikiwa kwamba kurejesha Ukhalifa ni miongoni mwa wajibu mkubwa wa dini hii kwa Sheikh Ali Bin Hajj.

4- Katika Sunan Abu Daud na ameisahihisha Albaani «ametuhadithia Ahmad Bin Swaleh ametuhadithia Asad Bin Musa ametuhadithia Muawiya Bin Swaleh amenihadithia Dhamra kwamba Ibn Zughb al-Ayadi amemuhadithia akasema alishuka juu yangu Abdullah Bin Hawala al-Azdi akasema kwangu: ametutuma Mtume wa Allah ‏ﷺ ili tupate ngawira kwa miguu yetu tukarudi hatukupata ngawira chochote na AKAJUA taabu katika nyuso zetu akasimama kwetu akasema: Ewe Allah usiwakabidhi kwangu nika dhaifu kuwatosheleza wala usiwakabidhi kwa nafsi zao wenyewe wakashindwa kuimudu wala usiwakabidhi kwa watu wakajichukulia wao kisha akaweka mkono wake juu ya kichwa changu au akasema juu ya utosi wangu kisha akasema: Ewe Ibn Hawala ukiona Ukhalifa umeshuka ardhi Takatifu hakika zimekaribia tetemeko na balaa na mambo makubwa, na Saa siku hiyo ni karibu zaidi kwa watu kuliko mkono wangu huu kwa kichwa chako, akasema Abu Daud Abdullah Bin Hawala ni Homsi»; na amesema Muslim: «ametuhadithia Huddab Bin Khalid al-Azdi ametuhadithia Hammad Bin Salama kutoka kwa Samak Bin Harb akasema: nimemsikia Jabir Bin Samura akisema: nimemsikia Mtume wa Allah ‏ﷺ akisema: "Uislamu utazidi kuwa mtukufu mpaka makhalifa kumi na wawili»; kutoka kwa al-Irbadh Bin Sariya akasema: «kisha akatupa mawaidha Mtume wa Allah ‏ﷺ siku moja baada ya Swala ya Alfajiri mawaidha yenye kufika sana macho yakabubujika na nyoyo zikaogopa, akasema mtu: Hakika haya ni mawaidha ya kuaga, basi unatuahidi nini kwetu ewe Mtume wa Allah? Akasema: ninakusieni kumcha Allah na kusikia na kutii hata kama mtumwa mweusi, kwani atakayeishi miongoni mwenu ataona tofauti nyingi, na tahadharini na mambo ya kuzua kwani ni upotevu, atakayelipata hilo miongoni mwenu basi ni juu yenu kushikamana na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa Waongofu waongozwa mshikamane nayo kwa magego»; Na amesimulia Muslim kutoka kwa Furat al-Qazzaz kutoka kwa Abu Hazim akasema: «nilikaa na Abu Huraira miaka mitano nikamsikia akihadithia kutoka kwa Mtume ‏ﷺ akasema "watu wa Israel walikuwa wanawaongoza Manabii kila alipokufa Nabii alifuatwa na Nabii na hakika hakuna Nabii baada yangu na watakuwepo Makhalifa watakuwa wengi wakasema basi unatuamrisha nini akasema timizeni bay'a ya wa kwanza kisha wa kwanza na wapeni haki yao kwani Allah atawauliza kuhusu yale aliyowachunga»; «utakuwepo Utume kwenu atakavyo Allah kuwepo, kisha ataunyanyua Allah atakavyo kuunyanyua, kisha utakuwepo Ukhalifa juu ya njia ya Utume, utakuwepo atakavyo Allah kuwepo, kisha ataunyanyua Allah atakavyo kuunyanyua, kisha utakuwepo ufalme wa kuumana, utakuwepo atakavyo Allah kuwepo, kisha ataunyanyua Allah atakavyo kuunyanyua, kisha utakuwepo ufalme wa kidhalimu, utakuwepo atakavyo Allah kuwepo, kisha ataunyanyua atakavyo kuunyanyua, kisha utakuwepo Ukhalifa juu ya njia ya Utume, kisha akanyamaza». Na hadithi hii ni nzuri ameitoa Ahmad (30/355 hadithi 18406), na al-Bazzar na al-Twabarani katika al-Awsat (6577) na sanad ya Ahmad ni nzuri ndani yake Daud Bin Ibrahim al-Wasiti amesimulia kutoka kwake al-Twyalisi na akamthibitisha na amemtaja Ibn Hibban katika wathika. Na ameisimulia hadithi pia al-Twyalisi na al-Baihaqi katika Minhaj al-Nubuwa, na al-Twabari, na hadithi ameisahihisha Albaani katika Silsila Sahihi, na ameihasanisha al-Arna'ut, na hadithi ina ushahidi kutoka kwa Safina radhi za Allah ziwe juu yake, akasema: Amesema Mtume wa Allah ﷺ: «UKHALIFA KATIKA UMMAT WANGU NI MIAKA THELATHINI, KISHA UFALME BAADA YA HAPO». KISHA AKASEMA SAFINA: SHIKILIA KWAKO UKHALIFA WA ABU BAKR, KISHA AKASEMA: NA UKHALIFA WA UMAR NA UKHALIFA WA UTHMAN, KISHA AKASEMA KWANGU: SHIKILIA UKHALIFA WA ALI akasema: TUKAPATA MIAKA THELATHINI. Ameisimulia Ahmad na amehusanisha al-Arna'ut. Na amesimulia Imamu Ahmad kutoka kwa Hudhaifa radhi za Allah ziwe juu yake kwamba alisema: "umeondoka Utume ukawepo Ukhalifa juu ya njia ya Utume". Na ameusahihisha al-Arna'ut.

More from null

Tafakuri Katika Kitabu: "Miongoni mwa Sifa za Kisaikolojia za Kiislamu" - Kipindi cha Kumi na Tano

Tafakuri Katika Kitabu: "Miongoni mwa Sifa za Kisaikolojia za Kiislamu"

Maandalizi ya Ustadhi Muhammad Ahmad Al-Nadi

Kipindi cha Kumi na Tano

Alhamdulillah, Mola Mlezi wa walimwengu, na sala na salamu zimwendee imamu wa wachamungu, na bwana wa mitume, aliyetumwa kuwa rehema kwa walimwengu, Bwana wetu Muhammad na ahli zake na masahaba zake wote, na tujaalie kuwa pamoja nao, na utukusanye katika kundi lao kwa rehema yako, Ee Mwenye kurehemu zaidi ya wote wanaorehemu.

Wasikilizaji wapendwa, wasikilizaji wa Radio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:

Assalamu alaykum warahmatullahi wabarakatuh, ama baada ya hayo: Katika kipindi hiki tunaendelea na tafakuri zetu katika kitabu: "Miongoni mwa Sifa za Kisaikolojia za Kiislamu". Na kwa ajili ya kujenga haiba ya Kiislamu, pamoja na kuzingatia akili ya Kiislamu na saikolojia ya Kiislamu, tunasema na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu: 

Enyi Waislamu:

Tulisema katika kipindi kilichopita: Pia ni sunna kwa Muislamu kumuombea ndugu yake kwa siri, kama ilivyo sunna kwake kumuomba ndugu yake amwombee, na ni sunna kwake kumtembelea na kuketi naye na kuendeleza uhusiano naye na kutoa mali yake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu baada ya kumpenda. Na ni vizuri kwa Muislamu kumlaki ndugu yake kwa yale anayopenda ili kumfurahisha kwa hayo. Na tunaongeza katika kipindi hiki kwa kusema: Hakika ni vizuri kwa Muislamu kumpa zawadi ndugu yake, kwa hadithi ya Abu Hurairah ambayo Bukhari ameitoa, katika Adab al-Mufrad, na Abu Ya'la katika Musnad yake, na al-Nasa'i katika Al-Kuna, na Ibn Abd al-Barr katika Al-Tamhid, na al-Iraqi alisema: Mnyororo wa wapokezi ni mzuri, na Ibn Hajar alisema katika Al-Talkhis al-Habir: Mnyororo wake wa wapokezi ni mzuri, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Peaneneni zawadi, mtapendana." 

Na ni vizuri pia kwake kuikubali zawadi yake, na kumlipa kwa zawadi hiyo, kwa hadithi ya Aisha kwa Bukhari, alisema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, alikuwa akipokea zawadi na kulipa kwa hiyo."

Na hadithi ya Ibn Omar kwa Ahmad na Abu Dawood na al-Nasa'i, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Yeyote anayeomba hifadhi ya Mwenyezi Mungu, basi mpeni hifadhi, na yeyote anayewaomba kwa jina la Mwenyezi Mungu, basi mpeni, na yeyote anayewaomba ulinzi wa Mwenyezi Mungu, basi mkingeni, na yeyote anayewafanyia wema, basi mlipe, na ikiwa hamupati, basi mwombeeni mpaka mjue kwamba mmemlipa."

Hii ni kati ya ndugu, na haina uhusiano wowote na zawadi za raia kwa watawala, kwani ni haramu kama rushwa, na miongoni mwa malipo ni kusema: Mwenyezi Mungu akulipe kheri. 

Tirmidhiy amepokea kutoka kwa Usama bin Zaid, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao, na akasema ni hadithi nzuri na sahihi, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Yeyote anayefanyiwa wema, na akamwambia aliyemfanyia: "Mwenyezi Mungu akulipe kheri", basi amekamilisha sifa." Na sifa ni shukrani, yaani malipo, hasa kutoka kwa mtu ambaye hapati chochote kingine, kama alivyopokea Ibn Hibban katika Sahih yake kutoka kwa Jabir bin Abdullah, alisema: Nilimsikia Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, akisema: "Yeyote anayefanyiwa wema, na hakupata wema wowote isipokuwa sifa, basi amemshukuru, na yeyote anayeuficha, basi ameukufuru, na yeyote anayejipamba kwa uongo, basi ni kama amevaa nguo mbili za uongo." Na kwa isnadi nzuri kwa Tirmidhiy kutoka kwa Jabir bin Abdullah, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Yeyote anayepewa zawadi, na akapata cha kulipa, basi alipe kwa hiyo, na ikiwa hapati, basi asifie kwa hiyo, kwa sababu yeyote anayesifia kwa hiyo, basi amemshukuru, na yeyote anayeuficha, basi ameukufuru, na yeyote anayejipamba kwa kile ambacho hakupatiwa, basi ni kama amevaa nguo mbili za uongo." Na kukufuru zawadi kunamaanisha kuificha na kuifunika. 

Na kwa isnadi sahihi, Abu Dawood na al-Nasa'i wamepokea kutoka kwa Anas, alisema: "Wahajiri walisema, Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu, Ansari wamechukua ujira wote, hatujawahi kuwaona watu wazuri zaidi katika kutoa kwa wingi, wala wazuri zaidi katika kuhurumiana katika uchache kuliko wao, na wametuondolea mzigo, alisema: Je, hamwawasifu kwa hilo na kuwaombea? Walisema: Ndio, alisema: Basi hiyo ni kwa hiyo." 

Na inampasa Muislamu kushukuru kidogo kama anavyoshukuru kingi, na kuwashukuru watu wanaomfanyia wema, kama alivyopokea Abdullah bin Ahmad katika Zawaid yake kwa isnadi nzuri kutoka kwa al-Nu'man bin Bashir, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Yeyote asiyeshukuru kidogo, hatashukuru kingi, na yeyote asiyewashukuru watu, hatamshukuru Mwenyezi Mungu, na kuzungumzia neema ya Mwenyezi Mungu ni shukrani, na kuiacha ni kufuru, na jamaa ni rehema, na utengano ni adhabu."

Na miongoni mwa sunna ni kumuombea ndugu yake kwa manufaa ya wema au kurahisisha magumu, kama alivyopokea Bukhari kutoka kwa Abu Musa, alisema: "Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, alikuwa ameketi pale alipokuja mtu akiuliza, au akihitaji haja, akatuelekeza uso wake na akasema ombeeni ili mthawabishwe na Mwenyezi Mungu atimize kwa ulimi wa nabii wake atakavyo."

Na kama alivyopokea Muslim kutoka kwa Ibn Omar kutoka kwa Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, alisema: "Yeyote aliyekuwa kiungo kwa ndugu yake Muislamu kwa mwenye mamlaka kwa manufaa ya wema au kurahisisha magumu, atasaidiwa kupita Siraati siku ya kuteleza miguu."

Na ni vizuri pia kwa Muislamu kulinda heshima ya ndugu yake kwa siri, kama alivyopokea Tirmidhiy na akasema hii ni hadithi nzuri kutoka kwa Abu al-Darda' kutoka kwa Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, alisema: "Yeyote anayerudisha (anayetetea) heshima ya ndugu yake, Mwenyezi Mungu atarudisha moto kutoka usoni mwake Siku ya Kiyama." Na hadithi hii ya Abu al-Darda' ameitoa Ahmad na akasema isnadi yake ni nzuri, na vile vile alisema al-Haythami. 

Na kama alivyopokea Ishaq bin Rahwayh kutoka kwa Asma binti Yazid, alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, akisema: "Yeyote anayetetea heshima ya ndugu yake kwa siri, ni haki kwa Mwenyezi Mungu kumwacha huru na moto." 

Na al-Quda'i ameitoa katika Musnad al-Shihab kutoka kwa Anas, alisema: Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Yeyote anayemsaidia ndugu yake kwa siri, Mwenyezi Mungu atamsaidia katika dunia na akhera." Na al-Quda'i pia ameitoa kutoka kwa Imran bin Hussein kwa ziada: "Naye anaweza kumsaidia." Na kama alivyopokea Abu Dawood na Bukhari katika Al-Adab al-Mufrad, na al-Zain al-Iraqi alisema: Isnad yake ni nzuri kutoka kwa Abu Hurairah kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: "Muumini ni kioo cha muumini, na muumini ni ndugu wa muumini, kokote anapokutana naye, anazuia kupotea kwake na anamzunguka nyuma yake."

Enyi Waislamu:

Mmejua kupitia hadithi za Nabii tukufu zilizotajwa katika kipindi hiki, na kipindi kilichopita, kwamba ni sunna kwa yule anayempenda ndugu yake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, kumjulisha na kumueleza upendo wake kwake. Na pia ni sunna kwa Muislamu kumuombea ndugu yake kwa siri. Kama ilivyo sunna kwake kumuomba ndugu yake amwombee. Na ni sunna kwake kumtembelea na kuketi naye na kuendeleza uhusiano naye na kutoa mali yake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu baada ya kumpenda. Na ni vizuri kwa Muislamu kumlaki ndugu yake kwa yale anayopenda ili kumfurahisha kwa hayo. Na ni vizuri kwa Muislamu kumpa zawadi ndugu yake. Na ni vizuri pia kwake kuikubali zawadi yake, na kumlipa kwa zawadi hiyo.

Na inampasa Muislamu kuwashukuru watu wanaomfanyia wema. Na miongoni mwa sunna ni kumuombea ndugu yake kwa manufaa ya wema au kurahisisha magumu. Na ni vizuri pia kwake kulinda heshima ya ndugu yake kwa siri. Je, hatutazifuata hukumu hizi za kisheria, na hukumu zingine za Uislamu; ili tuwe kama anavyopenda na kuridhika Mola wetu, mpaka abadilishe yaliyomo ndani yetu, na atengeneze hali zetu, na tupate ushindi wa kheri za dunia na akhera?! 

Wasikilizaji wapendwa: Wasikilizaji wa Radio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir: 

Tunatosheka na kiasi hiki katika kipindi hiki, tukitarajia kukamilisha tafakuri zetu katika vipindi vijavyo, InshaAllah Ta'ala, mpaka wakati huo na mpaka tukutane, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu na ulinzi wake na usalama wake. Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri na Assalamu alaykum warahmatullahi wabarakatuh. 

Fahamuni Enyi Waislamu! - Kipindi cha 15

Fahamuni Enyi Waislamu!

Kipindi cha 15

Kwamba miongoni mwa vyombo vya dola ya Khilafa ni wasaidizi, nao ni mawaziri ambao Khalifa huwateua pamoja naye, ili wamsaidie katika kubeba majukumu ya Khilafa, na kutekeleza majukumu yake, kwa sababu wingi wa majukumu ya Khilafa, haswa kila inapokua na kupanuka dola ya Khilafa, Khalifa hulemewa na kuyabeba peke yake, hivyo anahitaji mtu wa kumsaidia katika kuyabeba ili atekeleze majukumu yake, lakini haifai kuwaita mawaziri bila ya kizuizi mpaka isije ikachanganya maana ya waziri katika Uislamu ambayo ni sawa na msaidizi na maana ya waziri katika mifumo ya kidunia ya sasa kwa misingi ya kidemokrasia, kibepari, kilimwengu au mifumo mingine ambayo tunaishuhudia katika zama hizi za sasa.