Mfululizo wa "Ukhalifa na Uimamu katika Fikra ya Kiislamu"
na Mwandishi na Mfikiri Thair Salama – Abu Malik
Sehemu ya sitini na sita: Dhamana za kufikia Dola ya Kisheria kati ya Taswira ya Kiislamu na Taswira ya Kimagharibi – J2
Imeelezwa katika toleo la ishirini na tano la jarida la Al-Wa'i:
Utawala kwa mtazamo wa Magharibi: Ni kumiliki utashi na kumiliki utekelezaji. Iwapo utashi utanyang'anywa na uendeshaji wake kuwa mikononi mwa mwingine, mtu huyo aliyenyang'anywa utashi anakuwa mtumwa, na ikiwa anaendesha utashi wake mwenyewe, anakuwa bwana.
Ama mamlaka kwao ni: Utekelezaji wa utawala na hukumu. Na tofauti kati ya utawala na mamlaka ni kwamba utawala unajumuisha utashi na utekelezaji, yaani, unajumuisha uendeshaji wa utashi, na unajumuisha utekelezaji, wakati mamlaka inahusika tu na utekelezaji na haijumuishi utashi.
Ama kuhusu tofauti kati ya dhana ya mamlaka na utawala kwa mtazamo wa Magharibi, na dhana yake kwa mtazamo wa Waislamu, Magharibi ilifikia nadharia mbili za Utawala kwa taifa, na taifa ndio chanzo cha mamlaka baada ya mapambano makali yaliyokumba Ulaya katika Karne za Kati na kuendelea kwa karne kadhaa, ambapo ilikuwa ikitawaliwa na wafalme waliokuwa wakiwatumikisha watu chini ya mfumo wa nadharia ya Haki ya Kimungu ambayo ni: kwamba mfalme ana haki ya kimungu juu ya watu, na kwa mujibu wa haki hii ya kimungu, wafalme wanamiliki mamlaka, sheria na hukumu, na watu hawana haki katika mambo haya, na watu ni watumwa wasio na maoni wala utashi, lakini wao wanapaswa kutekeleza na kutii, na dhuluma na uonevu unaokumba taifa unatokana na kile ambacho wafalme wanafurahia cha haki ya kutunga sheria na haki ya mamlaka, hivyo watu walilalamika na mapinduzi yakaanzishwa na nadharia mbalimbali zikaibuka ili kuondoa nadharia ya Haki ya Kimungu na kuifuta kabisa, ndipo nadharia hizi mbili zikaibuka kwa mtazamo wa Magharibi. Na walifikia hitimisho kwamba watu wanapaswa kuendesha utashi wao wenyewe kwa sababu sio watumwa wa mfalme, lakini wao ni huru, na kwa kuwa watu ndio mabwana, basi wao ndio wanaomiliki sheria na utekelezaji, na wazo hili lilifanikiwa baada ya mapambano makali, na mabunge yakapatikana kuwakilisha taifa katika kutekeleza utawala, hivyo wakasema Baraza la Wawakilishi ni bwana wa nafsi yake, kwa hivyo nadharia ya utawala kwa taifa ina maana kwamba taifa linamiliki uendeshaji wa utashi wake na linamiliki utekelezaji wa utashi huu, na nadharia ya taifa ndio chanzo cha mamlaka ina maana kwamba taifa ndilo linamwakilisha mtawala juu yake ili atawale kwa jina lake, iwe mtawala ni mtekelezaji (mamlaka ya utendaji) au hakimu (mamlaka ya mahakama), wote wawili ni watawala na kila mmoja wao ni mamlaka.
Na kwa kuwa taifa linaweza kuendesha utashi, yaani, linaweza kutunga sheria, basi linatekeleza hilo lenyewe kupitia wawakilishi wake1, na kwa hivyo sheria inakuwa ya taifa, na kutoka hapa haisemekani kwamba taifa ndio chanzo cha sheria, lakini inasemwa kwamba sheria ni ya taifa kwa sababu ndilo linalotekeleza hilo lenyewe2. Ama mamlaka, taifa haliwezi kuitekeleza lenyewe kwa sababu hiyo haiwezekani kivitendo, na kutoka hapa mamlaka haikuwa ya taifa lakini mamlaka inatekelezwa na mtu mwingine isipokuwa taifa kwa uidhinishaji kutoka kwake, na kwa niaba yake, kwa hivyo lilikuwa ndilo chanzo cha mamlaka, yaani, ndilo linalompa mamlaka yule analiyemwakilisha, kama vile bwana anavyomwakilisha mtumwa wake, ili atekeleze kile anachotaka akitekeleze kulingana na utashi wake, na vile vile mtawala ikiwa ni pamoja na hakimu. Kwani yeye ni mwakilishi wa taifa na aliyeidhinishwa kutoka kwake kutekeleza mamlaka na hilo ni kulingana na utashi wake, yaani, kulingana na kile analotunga la sheria.
Na hali halisi hii ya taifa katika Magharibi kwa upande wa kuwa bwana wa nafsi yake inapingana na hali halisi ya taifa la Kiislamu, kwani taifa la Kiislamu limeamrishwa kuendesha matendo yake yote kwa hukumu za sheria, kwani Muislamu ni mja wa Mungu, hivyo haendeshi utashi wake wala hatekelezi kile anachotaka, lakini anaendesha utashi wake kwa amri za Mungu na makatazo yake, lakini yeye ndiye mtekelezaji, na kwa hivyo utawala sio wa taifa lakini ni wa sheria, ama utekelezaji ni wa taifa, na kwa hivyo mamlaka ilikuwa ya taifa.
Na kwa kuwa taifa haliwezi kutekeleza mamlaka lenyewe, kwa hivyo ni lazima kwake kumwakilisha anayetekeleza hilo kwa niaba yake.
Na sheria ilikuja na kubainisha jinsi ya kulitekeleza kwa njia ya bay'a na mfumo wa ukhalifa, kwa hivyo mamlaka ni ya taifa linateua kwa ridhaa yake anayetekeleza hilo kwa niaba yake, lakini kulingana na hukumu za sheria, yaani, sio kulingana na utashi wake lakini kulingana na sheria ya Mungu. Na kutoka hapa utawala ulikuwa wa sheria, na mamlaka ilikuwa ya taifa3. Mwisho
1- Na ni jambo la wazi sasa kwamba wazo kwamba wawakilishi wanatunga sheria kwa jina la taifa ni wazo ambalo halilingani na hali halisi na ni wazo la kupotosha, angalia katika kitabu hiki sura ya: Kutenganisha madaraka katika mfumo wa Magharibi, ambalo ni kanuni ambayo haipo katika hali halisi.
2- Miongoni mwa maadili ambayo demokrasia inasimamia na demokrasia inategemea kuwepo na kutokuwepo kwake: Kuamua maoni ya walio wengi katika jamii, na kuzuia mkusanyiko wa mamlaka mikononi mwa wachache, au unyonyaji wake, na uwakilishi wa mamlaka kwa maoni ya watu, na maadili haya matatu haiwezekani kuyafanikisha katika hali halisi, na mfumo mzima wa Magharibi unategemea mchanganyiko na kuingiliana kwa mamlaka na mkusanyiko wake mikononi mwa vyama tawala, na sheria zinatungwa na wachache wa wanazuoni wa sheria na mahakimu, na hairejelewi kwa watu isipokuwa katika sehemu ndogo sana yake, na mada ina maelezo mengi sana ambayo ni vigumu kuyaweka hapa, lakini demokrasia ni falsafa ya kufikirika ya kupotosha, haiwezekani kuwepo katika ardhi halisi!
3- Toleo la ishirini na tano la jarida la Al-Wa'i