Tafakuri katika Kitabu: "Miongoni mwa Misingi ya Saikolojia ya Kiislamu"
Kipindi cha Tisa
Himdi ni ya Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu, na sala na salamu zimwendee imamu wa wacha Mungu, na bwana wa mitume, aliyetumwa kama rehema kwa walimwengu, bwana wetu Muhammad, na kwa ahli zake na masahaba zake wote, na utufanye tuwe pamoja nao, na utukusanye katika kundi lao kwa rehema yako, Ee Mwingi wa rehema kuliko wote wenye kurehemu.
Wasikilizaji wapenzi, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:
Asalamu alaykum warahmatullah wabarakatuh, na baada ya hayo: Katika kipindi hiki tunaendeleza tafakuri zetu katika kitabu: "Miongoni mwa Misingi ya Saikolojia ya Kiislamu". Na kwa ajili ya kujenga utu wa Kiislamu, pamoja na kuzingatia akili ya Kiislamu na saikolojia ya Kiislamu, tunasema na kwa Mwenyezi Mungu ndio mafanikio yanatoka:
Enyi Waislamu:
Qur'ani Tukufu ni maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, aliyo teremsha kwa Mtume wake Muhammad صلى الله عليه وسلم kwa njia ya wahyi, Jibril a.s., kwa lafudhi na maana, tunamuabudu kwa kuisoma, yenye muujiza, iliyo nakiliwa kwetu kwa njia ya mutawatir. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {HAIMFIKII UONGO MBELE YAKE WALA NYUMA YAKE. NI UTEREMSHO UTOKAO KWA MWENYE HIKIMA, MWENYE KUSIFIWA}. (Fussilat 42) Imehifadhiwa kwa hifadhi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu pale aliposema: {HAKIKA SISI TUMETEREMSHA UKUMBUSHO, NA HAKIKA SISI NI WENYE KUULINDA}. (Al-Hijr 9)
Na Qur'ani enyi Waislamu: Nafsi huishi nayo, na nyoyo hutulia nayo, na watu hutoka katika giza kwenda kwenye nuru kwa idhini ya Mola wao Mlezi, kwenda kwenye njia ya Mwenye nguvu, Msifiwa. Qur'ani ndio zao kwa Muislamu, na zao gani hilo, na ni kwa mbeba da'wa muhimu zaidi na zaidi, nyoyo huijaa nayo, na mikono huimarika nayo, na mbeba da'wa huwa kama milima iliyo thabiti, dunia humdharau katika njia ya Mwenyezi Mungu, husema ukweli na haogopi lawama ya mwenye kulaumu katika njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo muumini ambaye anasukumwa na upepo kwa wepesi wake, anakuwa mzito zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko mlima wa Uhud, kwa sababu yeye ni msomaji wa Qur'ani, ulimi wake ni laini nayo, vidole vyake vinashuhudia.
Enyi Waislamu:
Hivyo ndivyo masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم walivyokuwa, wanatembea katika dunia, kana kwamba wao ni Qur'ani inatembea, wanatafakari aya zake, na wanazisoma kama inavyostahiki kusomwa, wanafanya kazi nayo na wanaialika, aya za adhabu zinawatikisa, na aya za rehema zinaeleza vifua vyao, macho yao yanatiririka machozi kwa unyenyekevu kwa muujiza wake na utukufu wake, na kukubali hukumu zake na hekima zake, wanaipokea kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم, basi aya zake zinakaa katika vilindi vya mioyo yao, kwa hivyo waliheshimika na kutawala, na walifurahi na kufaulu. Basi Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم alipo waaga kwenda kwenye urefu wa daraja, waliendelea kuitunza Qur'ani kama alivyowausia Mtume mwaminifu, sala na salamu za Mwenyezi Mungu zimwendee yeye na jamaa zake na masahaba zake wote. Basi wahifadhi wa Qur'ani walikuwa mstari wa mbele katika kuamrisha mema na kukataza maovu, na mbeba Qur'ani alikuwa wa kwanza katika kila jambo jema, na wa kwanza katika kuvamia kila jambo gumu katika njia ya Mwenyezi Mungu.
Enyi Waislamu:
Hakika inafaa kwa Waislamu kwa ujumla, na kwa wabebaji wa da'wa hasa, kwamba Qur'ani iwe ni chemchemi ya nyoyo zao, na iambatane na njia yao, iwaongoze kwenye kila jambo jema, na iwapandishe kutoka kilele hadi kilele, waitunze nyakati za usiku na pande za mchana, kwa kusoma na kuhifadhi na kufanya kazi nayo, ili wawe kweli ni warithi bora wa watangulizi bora.
Na hizi ni aya tukufu katika uteremshaji wa Qur'ani, na katika kuhifadhi kwake, na katika kuwa uongofu kwayo, na kheri kubwa ndani yake, na kutoka kwake na karibu yake: Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {AMEITEREMSHA ROHO MWAMINIFU JUU YA MOYO WAKO, ILI UWE MWENYE KUONYA}. (Ash-Shu'ara 194) Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {HAKIKA SISI TUMETEREMSHA UKUMBUSHO, NA HAKIKA SISI NI WENYE KUULINDA}. (Al-Hijr 9). Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {HAIMFIKII UONGO MBELE YAKE WALA NYUMA YAKE. NI UTEREMSHO UTOKAO KWA MWENYE HIKIMA, MWENYE KUSIFIWA}. (Fussilat 42). Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {HAKIKA HII QUR'ANI HUONGOZA KWENYE YALIYO SAWA KABISA, NA INAWABASHIRIA WAUMINI WANAO FANYA MEMA KWAMBA WATAPATA UJIRA MKUBWA}. (Al-Isra 9) Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {AMEKUFIKIENI MTUME WETU ANAKUELEZENI MENGI KATIKA YALE MLIYO KUWA MKIYAFICHA KATIKA KITABU, NA ANASAMEHE MENGI. HAKIKA AMEKUFIKIENI MWANGA NA KITABU KINACHO BABAINISHA KUTOKA KWA MWENYEZI MUNGU. MWENYEZI MUNGU ANAWAONGOZA KWENYE NJIA ZA AMANI WALE WALIO FUATA RADHI ZAKE, NA ANAWATOA KATIKA GIZA KWENDA KWENYE NURU KWA IDHINI YAKE, NA ANAWAONGOZA KWENYE NJIA ILIYO NYOOKA}. (Al-Ma'ida 16) Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {KITABU TUMEKITEREMSHA KWAKO ILI UWATOE WATU KATIKA GIZA WAINGIE KATIKA NURU KWA IDHINI YA MOLA WAO MLEZI, KWENYE NJIA YA MWENYE NGUVU, MWENYE KUSIFIWA}. (Ibrahim 1) Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:{JUU YA KUMKUMBUKA MWENYEZI MUNGU NYOYO HUTULIA}. (Ar-Ra'd 28) Na akasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: {HIVI HAWAITAFUTI MAANA YA QUR'ANI? LAU INGEKUWA INATOKA KWA ASIYE KUWA MWENYEZI MUNGU, BILA SHAKA WANGEKUTA NDANI YAKE MAKOSA MENGI}. (An-Nisa 82)
Na baada ya hayo enyi Waislamu: Hakika yaliyotangulia katika aya tukufu, yanaeleza nafasi kubwa ya Qur'ani Tukufu, na nafasi kubwa ya mbeba Qur'ani tukufu, ambaye anaibeba ili aitafakari na afanye kazi nayo, na aitunze katika hali zake zote, ili iwe ni nguvu kubwa katika njia zote za kheri, si kuiweka kwenye rafu mpaka vumbi imfunike, au kuipamba na kuifungia kwenye hazina zake mpaka isahaulike, na awe kwa hili anakuwa miongoni mwa wenye hasara, tunajikinga na Mwenyezi Mungu.
Basi itunzeni Qur'ani tukufu enyi ndugu wapenzi, na himeni kuisoma kama inavyostahiki kusomwa, na itafakarieni kama inavyostahiki kufikirika, na fanyeni kazi nayo kama inavyostahiki kufanywa kazi, na shikamaneni nayo kama inavyostahiki kushikamana, ili ladha yenu iwe nzuri, na harufu yenu iwe nzuri, na kwa hivyo muwe katika safu za mbele katika kubeba da'wa duniani, kama mtakavyokuwa katika safu za mbele peponi Akhera itakapo semwa: Soma na upande, kwa hayo mtakuwa mnafaa kupata ushindi mkubwa na mafanikio makubwa, na radhi kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni kubwa zaidi {NAWABASHIRIE WAUMINI}.
Wasikilizaji wapenzi: Wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:
Tunatosheka na kiasi hiki katika kipindi hiki, kwa kuwa tutakamilisha tafakuri zetu katika vipindi vijavyo inshaAllah Taala, basi mpaka wakati huo na mpaka tutakapokutana nanyi, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu na hifadhi yake na amani yake. Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri na Asalamu alaykum warahmatullah wabarakatuh.