Tafakari juu ya kitabu: "Miongoni mwa misingi ya Saikolojia ya Kiislamu"
Kipindi cha Kumi na Mbili
Himdi ni ya Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu, na sala na salamu zimwendee imamu wa wacha Mungu, na bwana wa mitume, aliyetumwa kama rehema kwa walimwengu, Bwana wetu Muhammad, na kwa ahli zake na masahaba zake wote, na tujaalie kuwa pamoja nao, na utufufue katika kundi lao kwa rehema yako, Ewe Mwenye kurehemu zaidi kuliko wote wenye kurehemu.
Wasikilizaji wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:
Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh, Ama baada ya hayo: Katika kipindi hiki tunaendelea na tafakari zetu katika kitabu: "Miongoni mwa misingi ya Saikolojia ya Kiislamu". Na kwa ajili ya kujenga utu wa Kiislamu, pamoja na kuzingatia akili ya Kiislamu na saikolojia ya Kiislamu, tunasema na kwa Mwenyezi Mungu ndio mafanikio:
Enyi Waislamu:
Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema, naye ndiye msema kweli zaidi: {Enyi mlio amini! Atakaye rudi nyuma miongoni mwenu, basi Mwenyezi Mungu atakuja leta watu anao wapenda nao wampenda, wanyenyekevu kwa Waumini, wenye nguvu juu ya makafiri, wanapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawaogopi lawama ya mlalamishi. Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mjuzi}. (Al-Maidah 54)
Katika aya tukufu kuna hotuba yenye sura ya onyo na ahadi, na maana yake: Enyi kundi la waumini, yeyote atakayerudi miongoni mwenu kutoka katika dini yake ya haki, na kuibadilisha na dini nyingine, na akarudi kutoka katika imani kwenda katika ukafiri, na katika aya kuna taarifa ya uasi wa baadhi ya Waislamu, kwa hiyo ni habari ya ghaibu kabla ya kutokea kwake, na makundi mengi yaliasi kutoka katika Uislamu, baadhi yao waliasi katika zama za Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani zimshukie, na baadhi yao katika zama za Abu Bakr, na Banu Hanifa, watu wa "Musailima mwongo" waliasi, na Musailima alimwandikia Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani zimshukie: "Kutoka kwa Musailima mjumbe wa Mwenyezi Mungu kwenda kwa Muhammad mjumbe wa Mwenyezi Mungu, ama baada ya hayo: Hakika ardhi nusu yake ni yangu na nusu yake ni yako". Akamjibu amani imshukie: «Kutoka kwa Muhammad mjumbe wa Mwenyezi Mungu kwenda kwa Musailima mwongo, ama baada ya hayo: Hakika ardhi ni ya Mwenyezi Mungu, humrithisha amtakaye katika waja wake, na mwisho mwema ni kwa wacha Mungu».
Kisha aya tukufu zikabainisha sifa za wale ambao Mwenyezi Mungu anawapenda. Mwenyezi Mungu amesema: {Basi Mwenyezi Mungu atakuja leta watu anao wapenda nao wampenda}. Yaani Mwenyezi Mungu ataleta mahali pa wale walioasi watu waumini ambao Mwenyezi Mungu anawapenda nao wampenda Mwenyezi Mungu. {Wanyenyekevu kwa Waumini, wenye nguvu juu ya makafiri}. Yaani wenye huruma na wanyenyekevu kwa waumini, wakali na wenye nguvu juu ya makafiri, Ibn Kathir amesema: Hizi ni sifa za waumini wakamilifu, kwamba mmoja wao awe mnyenyekevu kwa ndugu yake, mwenye nguvu juu ya adui yake kama alivyosema Mwenyezi Mungu: {Wakali kwa makafiri, wenye huruma wao kwa wao}. Na miongoni mwa alama za kumpenda Mwenyezi Mungu Mtukufu muumini ni kuwa mlaini, mnyenyekevu kwa ndugu zake waumini, aliyevaa vazi la heshima mbele ya makafiri na wanafiki. {Wanapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawaogopi lawama ya mlalamishi}. Yaani wanapigana jihadi kwa ajili ya kuinua neno la Mwenyezi Mungu, na hawajali wale wanaowalaumu, wao ni imara katika dini ya Mwenyezi Mungu, hawaogopi katika njia ya Mwenyezi Mungu mtu yeyote. {Hiyo ndiyo fadhila ya Mwenyezi Mungu humpa amtakaye}. Yaani yeyote anayesifika kwa sifa hizi njema, basi hiyo ni fadhila ya Mwenyezi Mungu kwake na ufanikishaji wake kwake. {Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wasaa Mjuzi}. Yaani Mwenye wasaa wa fadhila na ihsani, Mjuzi wa anayestahiki hayo.
Enyi Waislamu:
Kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake ni miongoni mwa mambo ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu ameyaunganisha na dhana ya kisheria ambayo ameifanya kuwa ni faradhi, na dalili juu ya hilo kutoka katika Sunnah zimeenea, miongoni mwazo ni hadithi ya Ka'ab bin Malik ndefu kuhusu wale watatu walioachwa nyuma kutoka Tabuk, na ndani yake Ka'ab anasema: «Ama mimi nilikuwa kijana zaidi na mwenye nguvu zaidi kati ya watu, nilikuwa natoka na kushuhudia sala pamoja na Waislamu na kuzunguka katika masoko, na hakuna mtu aliyekuwa ananizungumzia, na nilikuwa namjia Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie na kumsalimia naye yuko katika kikao chake baada ya sala, na nilikuwa nasema katika nafsi yangu: Je, ameziyumbisha midomo yake kujibu salamu yangu au la? Kisha nilikuwa nasali karibu naye na kumuibia macho, na nilipoelekea katika sala yangu alielekea kwangu, na nilipogeuka kumuelekea aliniepusha, mpaka iliponirefushia hilo katika ukatili wa watu, nilitembea mpaka nikapanda ukuta wa bustani ya Abu Qatada, naye ni mtoto wa ami yangu na mpendwa zaidi wa watu kwangu, nikamsalimia lakini wallahi hakunijibu salamu, nikasema: Ewe Abu Qatada nakuomba kwa Mwenyezi Mungu, je, unanijua nampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake? Akanyamaza, nikamrudia na kumuomba, akanyamaza, nikamrudia na kumuomba, akasema: Mwenyezi Mungu na Mtume wake ndio wanajua zaidi, macho yangu yakatiririka, na nikaondoka mpaka nikapanda ukuta...».
Na miongoni mwazo pia ni hadithi ya Sahl bin Saad, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: «Qutaiba bin Saeed ametuhadithia, Yaqub bin Abd al-Rahman ametuhadithia, kutoka kwa Abu Hazim, amesema Sahl bin Saad, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amenihabarisha kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie alisema siku ya Khaibar: Hakika nitampa bendera hii kesho mtu ambaye Mwenyezi Mungu atafungua kupitia mikono yake, anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanampenda. Amesema: Watu walikesha usiku wao wakijadiliana ni nani atakayepewa, watu walipoamka walimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie wote wanatarajia kupewa, akasema: Yuko wapi Ali bin Abu Talib? Ikasemwa: Yuko anaugua macho yake ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu. Akasema: Wamtumie mtu, akaletwa, Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie akamtemea mate machoni mwake na akamuombea, akapona mpaka kama vile hakuwa na maumivu, akampa bendera, Ali akasema: Ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nitapigana nao mpaka wawe kama sisi? Akasema: Nenda kwa utulivu mpaka ushuke katika uwanja wao, kisha uwaite kwenye Uislamu na uwahabarishe yale wanayopaswa kuwa nayo ya haki ya Mwenyezi Mungu ndani yake, basi wallahi Mwenyezi Mungu akimwongoza mtu mmoja kupitia wewe ni bora kwako kuliko kuwa na ngamia wekundu».
Tunasema enyi Waislamu:
Hakika kumpenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake ni miongoni mwa mambo ambayo Mwenyezi Mungu Mtukufu ameyaunganisha na dhana ya kisheria ambayo ameifanya kuwa ni faradhi, je, tumetekeleza faradhi hii kwa namna inayotakiwa kama walivyotekeleza masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie ili Mwenyezi Mungu atutukuze kwa ushindi wake kama alivyowatukuza, na atutukuze kwa dini yetu kama alivyowatukuza?
Wasikilizaji wapendwa: wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir:
Tunatosheka na kiasi hiki katika kipindi hiki, kwa kuwa tutakamilisha tafakari zetu katika vipindi vijavyo InshaAllah, mpaka wakati huo na mpaka tutakapokutana nanyi, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu na hifadhi yake na amani yake. Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri, na Assalamu alaikum warahmatullahi wabarakatuh.