Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani Wetu Jasiri Touqeer, Wahanga wa Kukosekana kwa Dola Mlezi
Mnamo siku ya Jumatatu iliyopita, Julai 21, 2025, ndege ya kivita ya aina ya (F-7 BGI) ya Jeshi la Anga la Bangladesh ilianguka katika jengo la sehemu ya msingi ya shule na chuo cha Milestone katika eneo la Uttara katika mji mkuu, kutokana na hitilafu ya kiufundi. Hii ilisababisha ajali mbaya ya kusikitisha, iliyoonyeshwa katika matukio ya kutisha ya watoto na wavulana walioungua na kukatwa viungo kati ya waliokufa na waliojeruhiwa.