Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani Wetu Jasiri Touqeer, Wahanga wa Kukosekana kwa Dola Mlezi

Mkasa wa Milestone: Watoto Wasio na Hatia na Rubani Wetu Jasiri Touqeer, Wahanga wa Kukosekana kwa Dola Mlezi

Mnamo siku ya Jumatatu iliyopita, Julai 21, 2025, ndege ya kivita ya aina ya (F-7 BGI) ya Jeshi la Anga la Bangladesh ilianguka katika jengo la sehemu ya msingi ya shule na chuo cha Milestone katika eneo la Uttara katika mji mkuu, kutokana na hitilafu ya kiufundi. Hii ilisababisha ajali mbaya ya kusikitisha, iliyoonyeshwa katika matukio ya kutisha ya watoto na wavulana walioungua na kukatwa viungo kati ya waliokufa na waliojeruhiwa.

Makubaliano Yanayoongezeka ya Kikoloni

Makubaliano Yanayoongezeka ya Kikoloni

Rais wa Marekani, Donald Trump, alipunguza rasmi ushuru wa forodha kwa bidhaa za Indonesia kutoka 32% hadi 19%. Makubaliano haya yalikuja baada ya mazungumzo ya haraka ya nchi mbili kati ya Trump na Rais wa Indonesia, Prabowo Subianto. Rais wa Indonesia alitangaza matokeo ya mawasiliano yake na Trump kuhusu kupunguzwa kwa ushuru wa forodha kwa bidhaa za Indonesia zinazouzwa Amerika mnamo Julai 16, 2025, na akasema: "Nimezungumza na Rais Donald Trump, na Alhamdulillah, ilikuwa ngumu sana. Hatimaye, tumefikia makubaliano.

Ulaya Yaitishia Iran: Makubaliano ya Nyuklia Kabla ya Tarehe Hii au (Snafu)!

Ulaya Yaitishia Iran: Makubaliano ya Nyuklia Kabla ya Tarehe Hii au (Snafu)!

Paris ilitangaza kuwa mawaziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Uingereza, Ujerumani na Umoja wa Ulaya walimjulisha mwenzao wa Iran Alhamisi 2025/7/18 nia yao ya kurejesha vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi yake ikiwa Iran haitafanya maendeleo katika kufikia makubaliano juu ya mpango wake wa nyuklia. Wizara ya mambo ya nje ya Ufaransa ilisema mawaziri wa Ulaya walimhakikishia Waziri wa Iran Abbas Araqji nia yao ya kutumia utaratibu wa (Snafu) ambao unaruhusu vikwazo vyote vya kimataifa dhidi ya Iran kurejeshwa ikiwa hakuna maendeleo yanayopatikana katika kufikia, ifikapo mwisho wa msimu wa joto, makubaliano juu ya mpango wa nyuklia wa Tehran. Kulingana na chanzo cha kidiplomasia cha Ufaransa, mawaziri wa mambo ya nje wa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani walimwomba waziri wa mambo ya nje wa Iran kurejea katika njia ya kidiplomasia.

Usiwe na Imani na Urafiki wa Urusi kwani Uadui wake kwa Uislamu Uko Wazi na Dhahiri

Usiwe na Imani na Urafiki wa Urusi kwani Uadui wake kwa Uislamu Uko Wazi na Dhahiri

Gazeti la kila siku la Al-Thawra lililochapishwa Sana'a siku ya Jumatatu, Julai 21, liliripoti habari yenye kichwa "Mazoezi ya Pamoja ya Uokoaji kati ya Iran na Urusi Leo katika Bahari ya Caspian," ambapo ilisema: "Mazoezi ya uokoaji wa baharini ya Casarex 2025, yanayoandaliwa na Jeshi la Wanamaji la Iran, yatafanyika katika Bahari ya Caspian kwa siku 3 kuanzia Jumatatu. Shirika la habari la Mehr la Iran liliripoti kwamba mazoezi ya pamoja ya uokoaji katika Bahari ya Caspian "Casarex 2025," yatafanyika kwa ushiriki wa meli kutoka Iran na Shirikisho la Urusi, kuanzia leo, na yataandaliwa na Meli ya Kaskazini ya Jeshi la Wanamaji la Iran."

203 / 10603