Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Jarida la Al-Raya: Ukweli wa kisiasa na kiitikadi uliothibitishwa na matukio ya umwagaji damu ya Suwayda

Jarida la Al-Raya: Ukweli wa kisiasa na kiitikadi uliothibitishwa na matukio ya umwagaji damu ya Suwayda

Mnamo 2025/7/16, kwa njia ya kushtua na ya ghafla, Wizara ya Ulinzi ya Syria ilitangaza kuanza kwa uondoaji wa vikosi vya jeshi la Syria kutoka mji wa Suwayda, baada ya makubaliano kati ya serikali na masheikh wa akili wa Druze na tangazo la Rais wa Syria kwa kipindi cha mpito Ahmed Al-Shara'a kuwateua makundi ya ndani na masheikh wa akili wa Druze kuwajibika kwa kudumisha usalama katika Suwayda, baada ya siku za mapigano makali ya umwagaji damu ambayo yalisababisha vifo vya mamia ya ndugu zetu mashahidi, baada ya wito wa Marekani wa kuondoka kwa vikosi vya serikali kutoka jimbo hilo,

Jarida la Al-Raya: Kupungua kwa nyota ya Amerika na kuchomoza kwa wazo la Khilafah

Jarida la Al-Raya: Kupungua kwa nyota ya Amerika na kuchomoza kwa wazo la Khilafah

Rais wa 47 wa Marekani, Donald Trump, alikuja madarakani kukabiliana na urithi uliokumbwa na migogoro ya ndani na nje, na changamoto kubwa zinazoikabili Marekani, muhimu zaidi ikiwa ni kuyumba kwa hadhi yake ya kimataifa. Hata hivyo, Trump, ambaye ni mtu mkaidi, anayejiamini, anayejua kupambana na kushindana na hakati tamaa, kiasi kwamba aliwatisha wapinzani wake na akajilazimisha kuongoza chama, na sasa anarejea kwa mara ya pili Ikulu ya White House akiwa na nguvu, akiwa amejihami na ushindi mkubwa dhidi ya mgombea wa chama cha Democratic, Kamala Harris, na akiungwa mkono na makampuni makubwa ya kibepari, yakiwa na sehemu zake mbili za ubepari wa kawaida, unaowakilishwa na makampuni ya mafuta, silaha na reli,

Kushi News: Taarifa kwa Vyombo vya Habari Serikali ya "Matumaini" Yageuka kuwa Jinamizi kwa Maisha ya Watu kwa Kuporomoka kwa Thamani ya Pauni!

Kushi News: Taarifa kwa Vyombo vya Habari Serikali ya "Matumaini" Yageuka kuwa Jinamizi kwa Maisha ya Watu kwa Kuporomoka kwa Thamani ya Pauni!

Katika hotuba yake baada ya kuapishwa kama Waziri Mkuu, Kamel Idris alisema: "Kauli mbiu yetu ni matumaini na ujumbe ni kufikia usalama, ustawi, na maisha mazuri kwa kila raia wa Sudan!" Katika taarifa yake ya kwanza kwa vyombo vya habari, alisema atajitolea muda wake na juhudi zake ili kufikia maisha yenye heshima kwa kila Msudan. Na tunaingia mwezi wa tatu, na baraza lake la mawaziri halijakamilika hadi sasa, na matumaini ambayo aliahidi watu yamegeuka kuwa jinamizi la kutisha, lilianza na kuporomoka kwa pauni ya Sudan dhidi ya sarafu zingine, haswa dola, ambapo soko sambamba (nyeusi) lilishuhudia ongezeko kubwa, ambapo dola moja ilizidi kizingiti cha pauni elfu 3 za Sudan,

Rada: Kuzimika kwa Nyota ya Amerika na Kuchomoza kwa Wazo la Ukhalifa. Imeandikwa na Mwanasheria/ Hatem Jaafar (Abu Awab)

Rada: Kuzimika kwa Nyota ya Amerika na Kuchomoza kwa Wazo la Ukhalifa. Imeandikwa na Mwanasheria/ Hatem Jaafar (Abu Awab)

Rais wa 47 wa Marekani, Donald Trump, alikuja madarakani kukabiliana na urithi uliokumbwa na migogoro ya ndani na nje, na changamoto kubwa zinazoikabili Marekani, muhimu zaidi ikiwa ni kuyumba kwa hadhi yake ya kimataifa. Hata hivyo, Trump, ambaye ni mtu mkaidi, anayejiamini, anayefahamu mapambano na migogoro na hatakata tamaa, kiasi kwamba aliwatisha wapinzani wake na kujilazimisha kuongoza chama, na sasa anarejea kwa mara ya pili Ikulu ya White House kwa nguvu, akiwa na ushindi mkubwa dhidi ya mgombea wa chama cha Democratic Kamala Harris, na akisaidiwa na makampuni makubwa ya kibepari, katika sehemu zake mbili za ubepari wa kawaida unaowakilishwa na kampuni za mafuta, silaha na reli,

Jarida la Ar-Raya: Ushuru wa Forodha kama Njia ya Shinikizo la Kimkakati, Mvutano Baridi kati ya Marekani na China, na Changamoto ya BRICS

Jarida la Ar-Raya: Ushuru wa Forodha kama Njia ya Shinikizo la Kimkakati, Mvutano Baridi kati ya Marekani na China, na Changamoto ya BRICS

Nchi kumi na moja wanachama wa kundi la BRICS (Brazil, Urusi, India, China, Afrika Kusini, Misri, Ethiopia, Iran, Indonesia, Saudi Arabia, na Falme za Kiarabu) walikutana Rio de Janeiro, mji mkuu wa Brazil siku ya Jumamosi, Julai 6, 2025, ambapo washiriki walitia saini hati yenye kichwa "Kuimarisha Ushirikiano kati ya Nchi za Kusini kwa Utawala Jumuishi na Endelevu zaidi" ambayo inasisitiza dhamira ya kundi hilo la kukuza ushirikiano wa pande nyingi, kutetea sheria za kimataifa, na kutafuta mfumo wa kimataifa ulio sawa zaidi. Katika mkutano huu, hakuna maamuzi au miradi iliyochukuliwa kuhusiana na utoaji wa mfumo mpya wa fedha,

Jarida la Al-Raya: Öcalan na Kuharakisha Chama chake Kuacha Silaha

Jarida la Al-Raya: Öcalan na Kuharakisha Chama chake Kuacha Silaha

Neno lililo katika picha lilichapishwa tarehe 2025/7/9 kutoka kwa kiongozi wa chama cha Wafanyakazi wa Kikurdi, Abdullah Öcalan, akiahidi kuharakisha mchakato wa chama chake kuacha silaha, akisema: "Katika muktadha wa kutimiza ahadi tulizoahidi, utaratibu wa kuweka chini silaha unapaswa kuanzishwa ambao unachangia maendeleo katika mchakato, kukomesha mapambano ya silaha kwa hiari na mpito kwa hatua ya kisheria na siasa za kidemokrasia."

Jarida la Al-Raya: Mustakabali wa Vita vya Kisasa na Jukumu Lililopotea la Ukhalifa

Jarida la Al-Raya: Mustakabali wa Vita vya Kisasa na Jukumu Lililopotea la Ukhalifa

Vita vinavyoendelea katika sehemu mbalimbali za dunia, hasa vita kati ya Urusi na Ukraine na mgogoro kati ya Iran na shirika la Kiyahudi, vinaonyesha wazi kwamba dunia imeingia katika awamu mpya na tofauti ya vita vya kijeshi na kiintelijensia. Mtazamo wa kizamani wa vita, unaotegemea majeshi makubwa ya miguu, vifaru, na mizinga, unabadilika na unaporomoka kwa kasi. Leo, mataifa kama Marekani, China, na Urusi yanatenga bajeti kubwa kwa ajili ya viwanda vya kijeshi vya hali ya juu, na yanaendelea kufafanua upya mbinu mpya za vita. Mapambano katika medani za kisasa hayategemei tena risasi na bunduki,

Jarida la Ar-Raya: Itikadi ya Kiislamu ndio msingi wa wokovu na dira ya maisha

Jarida la Ar-Raya: Itikadi ya Kiislamu ndio msingi wa wokovu na dira ya maisha

Itikadi kwa lugha ni kile kinacho fungamana moyoni, na katika sheria ni kuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho na Qadar kheri yake na shari yake, kama ilivyokuja katika Sahih mbili kutoka kwa Omar bin Al-Khattab kwamba mtu alikuja kwa Nabii ﷺ akimuuliza na kumsadikisha mpaka akasema: NIJULISHE KUHUSU IMANI? Akasema: «UAMINI KWA MWENYEZI MUNGU NA MALAIKA WAKE NA VITABU VYAKE NA MITUME WAKE NA SIKU YA MWISHO NA UAMINI QADAR KHERI YAKE NA SHARI YAKE».

205 / 10603