Jarida la Al-Raya: Ukweli wa kisiasa na kiitikadi uliothibitishwa na matukio ya umwagaji damu ya Suwayda
Mnamo 2025/7/16, kwa njia ya kushtua na ya ghafla, Wizara ya Ulinzi ya Syria ilitangaza kuanza kwa uondoaji wa vikosi vya jeshi la Syria kutoka mji wa Suwayda, baada ya makubaliano kati ya serikali na masheikh wa akili wa Druze na tangazo la Rais wa Syria kwa kipindi cha mpito Ahmed Al-Shara'a kuwateua makundi ya ndani na masheikh wa akili wa Druze kuwajibika kwa kudumisha usalama katika Suwayda, baada ya siku za mapigano makali ya umwagaji damu ambayo yalisababisha vifo vya mamia ya ndugu zetu mashahidi, baada ya wito wa Marekani wa kuondoka kwa vikosi vya serikali kutoka jimbo hilo,