Jimbo la Tunisia: Maombolezo ya Mbeba Da'wa, Ustadh Hassan Nower
Hizb ut Tahrir katika jimbo la Tunisia inamuomboleza mmoja wa wanaume wake kutoka kwa wabebaji da'wa, Ustadh Hassan Nower, ambaye amefariki dunia leo Ijumaa, tarehe 24 Dhul-Hijjah 1446 Hijria, sawa na 2025/6/20 Miladia, baada ya kuugua kwa muda mrefu, ugonjwa uliomlemesha mwili wake lakini haukuzima mwenge wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi katika safu za wafanyakazi wa kurejesha maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume.