Radaa: Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan "Ibrahim Uthman Abu Khalil" katika mahojiano motomoto kuhusu hali ya sasa ya kisiasa
Hizb ut-Tahrir jimbo la Sudan ni miongoni mwa vyama vya kisiasa vyenye shughuli nyingi hata wakati wa vita, hivyo ni mfuatiliaji mzuri wa matukio na ina mtazamo ambao haufichi, watu hukubaliana nayo au hawakubaliani nayo, na wakati kazi ilipokwama Khartoum kutokana na vita, chama kilihamia Port Sudan, mji mkuu wa utawala, na kukodi ofisi ambayo iliendelea na shughuli zake kupitia hiyo. "Radaa News" ilikuwa na mahojiano haya na Ustadh Ibrahim Uthman Abu Khalil, msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan, kwa ajili ya kumbukumbu za mazungumzo.