Kujiunga waziwazi na Muungano wa Kimataifa wa Kupambana na "Ugaidi" ni kujitenga na misingi na kuteleza hatari kuelekea kuzimu
Waziri wa Habari wa Syria, Hamza Al-Mustafa, alisisitiza "Syria hivi karibuni imesaini tamko la ushirikiano wa kisiasa na Muungano wa Kimataifa wa kushinda Daesh," na kwamba "Syria ni mshirika katika kupambana na ugaidi," na akaongeza: "Rais Trump alisifu mabadiliko ya Syria na alionyesha kuunga mkono kwake mpango unaowezekana wa usalama na (Israel)." Wakati huo huo, Trump aliwaambia waandishi wa habari, baada ya kukutana na Rais wa Syria wa kipindi cha mpito, Ahmed Al-Sharaa, katika Ikulu ya White House, kwamba alikuwa na makubaliano na Al-Sharaa, na kwamba alikuwa na imani na hakika kwamba ataweza kutekeleza majukumu yake na kazi yake kwa mafanikio, na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilisifu Ijumaa iliyopita kile ilichokiita "maendeleo makubwa" katika tabia ya uongozi mpya wa Syria.