Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Muhtasari wa Habari 07-08-2025

Muhtasari wa Habari 07-08-2025

Shirika la Kiyahudi lilitishia kukalia kabisa Ukanda wa Gaza. Mnamo 2025/8/5, ilitangazwa kuwa Waziri Mkuu wake, Netanyahu, alifanya mashauriano kuhusu suala hili na atatangaza uamuzi kuhusu hilo baadaye. Ikumbukwe kwamba kwa miezi 22 amekuwa akifanya kazi ya kuharibu eneo hilo na kuangamiza watu wake, kwani ameharibu zaidi ya 80% ya nyumba, shule na hospitali zao, na anaendelea kuwashambulia watu katika mahema, mitaani, na karibu na vituo vya ugawaji wa misaada. Yeye na jeshi lake hawajashiba damu ya watu wa Gaza.

Enyi Waislamu: Je, bado mna matumaini kwa watawala wenu wajinga?!

Enyi Waislamu: Je, bado mna matumaini kwa watawala wenu wajinga?!

Bado shirika la Kiyahudi linaendelea na uhalifu wake dhidi ya watu wa Gaza, na kusababisha makumi ya mashahidi kuongezeka kila siku, na pia linaendelea kuweka mzingiro Gaza, na watu wake wanakufa kwa njaa, na wamekuwa bila chakula, kinywaji, dawa, au makazi, licha ya majaribio fulani ya kupeleka msaada kwao kwa aibu! Lakini mamia ya maelfu hawapati hata tonge la kujikimu au kutuliza njaa za watoto wao, hivyo wanakuwa wanakufa kwa njaa mikononi mwao na mbele ya macho ya dunia nzima bila msaidizi au mlinzi.

177 / 10603