Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Sudan: Janga la Karne Lililofichwa Machoni pa Ulimwengu

Sudan: Janga la Karne Lililofichwa Machoni pa Ulimwengu

Dola ya Kiislamu, mlinzi wa raia wake, haipo, na Waislamu wanaishi katika dhiki, mateso na majanga katika sehemu mbalimbali za dunia, ikiwa ni pamoja na Sudan, ambayo kwa sasa inakabiliwa na mojawapo ya majanga mabaya zaidi ya kibinadamu katika historia ya kisasa kutokana na mapigano ya umwagaji damu yanayoendelea kwa miaka miwili kati ya jeshi na vikosi vya msaada wa haraka, ambayo yamesababisha majanga ya kutisha ambayo hakuna mtu anayezungumzia au kujaribu kuyazuia. Vita vilivyosahaulika ambavyo vyombo vya habari havitoi mwanga wowote, na hakuna nchi au taasisi zinazofichua mambo yake ya ndani.

Uhalifu katika Nchi Hutokomezwa kwa Kutumia Adhabu za Kisharia

Uhalifu katika Nchi Hutokomezwa kwa Kutumia Adhabu za Kisharia

Matukio ya uhalifu wa unyang'anyi, uporaji na wizi yanaendelea (tisa ndefu); ambao huwatishia wapita njia katika barabara za umma kwa silaha na kuwanyang'anya pesa zao na kuwashambulia, na hurudiwa asubuhi na jioni katika eneo la Al-Kalakla Al-Wahda kusini mwa Khartoum, mji mkuu, na katika miji mingi ya Sudan. Wiki iliyopita, mtu alishambuliwa na kutishiwa kwa silaha, na simu yake iliporwa, huku kila mtu akishangaa, kisha wakakimbia kwa pikipiki, kisha wakaenda kwenye barabara nyingine na kumpora na kumshambulia mtu wa pili, na wa tatu.

178 / 10603