Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Jarida la Ar-Raya: Vita vya Mauaji ya Kimbari Gaza Vinaendelea na Misaada ni Mitego ya Kifo

Jarida la Ar-Raya: Vita vya Mauaji ya Kimbari Gaza Vinaendelea na Misaada ni Mitego ya Kifo

Viongozi wa Kiyahudi hawakuficha nia zao dhidi ya Ukanda wa Gaza tangu siku za mwanzo za vita, iwe kupitia matamko yao au kupitia mashine yao ya uhalifu ya vita. Kuondoa Gaza ya wakaazi wake, na kuwahamisha watu wake kutoka kwake bado ni lengo ambalo shirika la Kiyahudi linatafuta kulitimiza kwa nguvu, na linategemea katika jitihada zake hizi za kishetani msaada wa kisiasa na kifedha wa Magharibi na haswa kutoka Amerika, na pia inategemea ushirikiano kutoka kwa watawala wote wa Waislamu, haswa watawala wa kile kinachoitwa nchi zinazozunguka, na matamko yote yanayotoka kwao yakidai kukataa uhamaji ni uwongo mtupu.

Jarida la Ar-Raya: Mgogoro wa kiafya Sudan unahitaji mfumo unaoshughulikia masuala ya watu na kuwahurumia

Jarida la Ar-Raya: Mgogoro wa kiafya Sudan unahitaji mfumo unaoshughulikia masuala ya watu na kuwahurumia

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu imetangaza kuwa Sudan inakabiliwa na mgogoro mkubwa wa kiafya, ambapo 65% ya watu hawana huduma za kutosha za kiafya, huku watoto wakiwa 55% ya wanaohitaji msaada na wanaendelea kuwa hatarini zaidi kwa milipuko ya magonjwa. Ofisi hiyo ilisisitiza kuwa kati ya 70 na 80% ya vituo vya afya katika maeneo yenye migogoro havifanyi kazi. Ofisi hiyo ilionya kuwa mamilioni ya Wasudan wanateseka, ikisisitiza haja ya jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka ili kuepusha janga kubwa zaidi la kibinadamu. (Al-Sharq - Sudan, 2025/6/23).

Jarida la Al-Raya: Viongozi wa Pakistan walivyopoteza heshima yao mbele ya India na Trump?!

Jarida la Al-Raya: Viongozi wa Pakistan walivyopoteza heshima yao mbele ya India na Trump?!

Baada ya viongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan kupoteza ushindi ambao tai wa jeshi la anga la Pakistan na simba wa jeshi walipata dhidi ya India mwezi uliopita, na kuipa India somo ambalo haitawahi kulisahau, kwa kukubali kusitisha mapigano kati ya nchi hizo mbili, huku India ikisisitiza kusitisha utekelezaji wa mkataba wa maji na kunyima Pakistan takriban 80% ya maji yanayoingia kutoka Mto Indus - ambao unaanzia Uchina na kupitia India kisha Pakistan - na India kuendelea kukalia Kashmir..

Jarida la Ar-Raya: Sheria ya zamani ya upangaji nchini Misri kati ya ukosefu wa uangalizi na kujitolea kwa manufaa na tabaka

Jarida la Ar-Raya: Sheria ya zamani ya upangaji nchini Misri kati ya ukosefu wa uangalizi na kujitolea kwa manufaa na tabaka

Katika hatua ambayo Bunge la Misri liliielezea kama ya kihistoria, Baraza la Wawakilishi liliidhinisha katika kikao cha Jumatano, Julai 2, 2025, mswada wa sheria ya zamani ya upangaji na kupanga upya uhusiano kati ya mwenye nyumba na mpangaji, baada ya miaka mingi ya mabishano na mzozo kati ya maslahi ya wamiliki na wapangaji. Lakini yeyote anayeangalia sheria hii kwa jicho la Kiislamu, na kuipima kwa kipimo chake sio kwa kipimo cha kibepari, anatambua kuwa kilichotokea sio mageuzi, lakini badala yake ni uthibitisho wa njia potofu ambayo inatawala mfumo wa kibinadamu usio wa haki na kupoteza haki ya uangalizi wa kisheria ambayo Uislamu umeamuru kwa serikali.

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 555

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 555

Enyi Waislamu: Hawa hapa watawala wenu wamejitokeza katika uhalisia wao, na imewadhihirikia kuwa wao wana hamu na maslahi ya maadui zenu na si maslahi yenu, bali wao wako tayari kuwatoa nyinyi kama kafara kwa maadui zenu kwa ajili ya kulinda viti vyao ambavyo nguzo zake zimepinda, na Gaza ni ushahidi mzuri, na hii hapa Iran imejitokeza mbele ya macho yenu, na imetanguliwa na Somalia, Iraq, Yemen, Libya na Syria, basi mnafanya nini, na mpaka lini mtabaki kimya juu yao?!

231 / 10603