Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Jarida la Al-Raya: Kutoka Nile hadi Bwawa ni vita vya umma si vita vya mfumo

Jarida la Al-Raya: Kutoka Nile hadi Bwawa ni vita vya umma si vita vya mfumo

Uwanja wa Afrika siku hizi unashuhudia kuongezeka kwa mvutano mpya na lawama za pande zote kati ya Misri na Ethiopia kutokana na wimbi la mafuriko yaliyokumba maeneo makubwa nchini Sudan na sehemu za Misri, na kufuatiwa na lawama za wazi za Misri kwa Ethiopia kwa kusababisha mafuriko haya kupitia uendeshaji au umwagiliaji wa maji ya Bwawa la Renaissance kwa upande mmoja na bila uratibu, wakati Ethiopia ilipoharakisha kukanusha wajibu wake na kuzingatia lawama hizo kuwa "madai ya kupotosha," ikisisitiza kwamba sababu kuu ni mvua kubwa za msimu katika nyanda za juu za Ethiopia.

Jarida la Al-Raya: Syria Mpya na Vita dhidi ya Uislamu wa Kisiasa

Jarida la Al-Raya: Syria Mpya na Vita dhidi ya Uislamu wa Kisiasa

 Imekuwa wazi kwa kila mwangalizi anayefahamu siasa za kimataifa na kikanda katika eneo la Mashariki ya Kati kwamba kinachoendelea Syria kinafanyika katika muktadha wa mpango kamili wa Amerika katika eneo hilo. Mpango huu ulikuwa na vikwazo mbele yake na Amerika imekuwa ikifanya kazi ya kuondoa vikwazo hivyo tangu matokeo ya operesheni ya Mvua Kubwa ya Al-Aqsa na yaliyofuata, kuanzia uharibifu wa Gaza na jaribio la kuondoa nguvu ya kijeshi ya Hamas, na uharibifu wa nguvu ya kijeshi ya Hezbollah ya Iran huko Lebanon na Syria, na kulipua mpango wa nyuklia nchini Iran yenyewe. Na hapo awali, Amerika ilikuwa imemshirikisha Urusi katika vita vya Ukraine. 

Jarida la Ar-Raya: Kati ya Dhahabu na Dola

Jarida la Ar-Raya: Kati ya Dhahabu na Dola

Amerika, katika enzi ya Rais Nixon, ilichukua hatua ya kufuta makubaliano ya Bretton Woods mnamo 1971/8/15 kuhusu kuweka bei ya dhahabu kuwa dola 35 kwa aunsi moja ya dhahabu. Sababu kuu ya uamuzi huo wa kihistoria ilikuwa ni ongezeko kubwa la idadi ya dola zilizotolewa na Benki Kuu, hasa fedha hizo ambazo Amerika ilitenga kwa ajili ya kuokoa Ulaya, ambazo zilijulikana kama Mpango wa Marshall. Ulaya ilikuwa imekusanya takriban dola bilioni 10-40 kufikia mwaka 1971, ambazo thamani yake kwa dhahabu, kulingana na makubaliano ya Bretton Woods, ilikuwa tani 11.2-40.8 za dhahabu.

Jarida la Ar-Raya: Matukio ya Gaza na Syria yamefichua udanganyifu na kuthibitisha ukweli

Jarida la Ar-Raya: Matukio ya Gaza na Syria yamefichua udanganyifu na kuthibitisha ukweli

Tangu tarehe saba ya Oktoba 2023, Gaza ilianza kuandika kwa damu yake na vipande vya miili ya watoto wake kisa cha ushujaa mkuu kabisa katika kukabiliana na ukatili, ikiikabili taasisi ya Kiyahudi iliyojaa silaha na msaada wa Magharibi, na juu yake msaada wa moja kwa moja na wa jeuri wa Marekani. Mapambano hayakuwa sawa katika vifaa, lakini yalikuwa bora katika itikadi, hivyo Gaza ilishusha hadhi ya jeshi lisiloshindwa, na kufichua uongo wa nguvu ambayo vyombo vya habari vya Magharibi vilikuwa vikieneza kwa uadui na vyombo vya habari rasmi katika nchi yetu kwa unyenyekevu na udhalili, na kufichua kwamba hawawezi kushindwa sio sifa ya kweli ya adui mwoga,

Jarida la Ar-Raya: Mseto wa Ar-Raya – Toleo la 571

Jarida la Ar-Raya: Mseto wa Ar-Raya – Toleo la 571

Mradi wa Hizb ut-Tahrir wa kusimamisha Khilafah Rashidah siyo tu mtazamo wa kinadharia, bali ni mradi kamili wa kistaarabu unaotegemea wahyi, na unawapa wanadamu mbadala wa ustaarabu wa kimada wa Magharibi ambao umethibitisha kushindwa kwake katika kufikia furaha na utulivu. Wakati huo huo, ni mradi wa kivitendo ulio tayari kutekelezwa, iwapo utapatikana utashi wa kisiasa miongoni mwa Ummah, na nguvu zake na majeshi yake yatahamasika kuusimamisha.

33 / 10603