Habari na Maoni

Usiwe na Imani na Urafiki wa Urusi kwani Uadui wake kwa Uislamu Uko Wazi na Dhahiri

Usiwe na Imani na Urafiki wa Urusi kwani Uadui wake kwa Uislamu Uko Wazi na Dhahiri

Gazeti la kila siku la Al-Thawra lililochapishwa Sana'a siku ya Jumatatu, Julai 21, liliripoti habari yenye kichwa "Mazoezi ya Pamoja ya Uokoaji kati ya Iran na Urusi Leo katika Bahari ya Caspian," ambapo ilisema: "Mazoezi ya uokoaji wa baharini ya Casarex 2025, yanayoandaliwa na Jeshi la Wanamaji la Iran, yatafanyika katika Bahari ya Caspian kwa siku 3 kuanzia Jumatatu. Shirika la habari la Mehr la Iran liliripoti kwamba mazoezi ya pamoja ya uokoaji katika Bahari ya Caspian "Casarex 2025," yatafanyika kwa ushiriki wa meli kutoka Iran na Shirikisho la Urusi, kuanzia leo, na yataandaliwa na Meli ya Kaskazini ya Jeshi la Wanamaji la Iran."

Gaza Licha ya Tishio la Njaa Bado Inazidi Kumlemea Adui, Je, Kisingizio cha Watu wa Nguvu Ni Kipi?

Gaza Licha ya Tishio la Njaa Bado Inazidi Kumlemea Adui, Je, Kisingizio cha Watu wa Nguvu Ni Kipi?

Al-Sharq Al-Ikhbariya iliripoti jioni ya 2025/7/21 habari mbili kuhusu Gaza; ya kwanza ilikuwa na kichwa: "Magari ya uvamizi yamerusha mabomu ya mwanga katika anga ya Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza, kufuatia kuanguka kwa kikosi cha Israel katika shambulio la kuvizia." Na ya pili ilikuwa na kichwa: "Mashahidi na majeruhi katika uvamizi wa adui uliowalenga wanaosubiri misaada katika Roundabout ya Nabulsi magharibi mwa Gaza."

9 / 1315