Wanawake Lazima Watambue Udanganyifu wa Utofauti na Ujumuishaji katika Siasa za Uliberali
Kituo cha televisheni cha Al-Islam kimejadili ripoti mpya inayofichua mifumo ya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na ubaguzi wa kitaaluma unaowaathiri wanawake Waislamu katika vyombo vya habari. Athari hii imeenea hadi masuala ya afya ya akili na imani kwa taasisi. Ripoti ilijadili jinsi mtazamo wa waandishi wa habari wanawake Waislamu unaathiriwa hasa na ukiukwaji mdogo, dhana potofu na tofauti za mishahara.