Gaza Kati ya Kuzingirwa Kikatili, Njaa ya Kimfumo, na Wajibu wa Kisharia kwa Umma na Majeshi Yake
Tangu Oktoba 2023, Gaza inaishi moja ya majanga makubwa ya kibinadamu katika enzi ya kisasa, ambapo zaidi ya watu milioni mbili wamezingirwa, wakiachwa kuwa mawindo ya njaa, kiu, ugonjwa na uharibifu. Ripoti za Umoja wa Mataifa na Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka na mashirika mengine ya kibinadamu zinathibitisha kwamba wakaazi wa Gaza wanakabiliwa na njaa kubwa, huku vifo vya watoto vikiripotiwa kutokana na utapiamlo na upungufu wa maji mwilini, na ukosefu wa dawa na chakula.