Machapisho ya Hivi Karibuni

Makala Iliyoangaziwa

null

null

Soma zaidi
Jarida la Ar-Raya: Ushawishi wa China unaongezeka nchini Kyrgyzstan

Jarida la Ar-Raya: Ushawishi wa China unaongezeka nchini Kyrgyzstan

Kyrgyzstan inazidi kuwa chini ya sera ya upanuzi ya China siku baada ya siku, kama inavyothibitishwa na idadi ya makubaliano na miradi mikubwa kati ya nchi hizo mbili. Mnamo Oktoba 21, 2025, Shirika la Kitaifa la Uwekezaji chini ya Urais wa Kyrgyz lilitangaza utiaji saini wa hati ya makubaliano na kampuni ya Kichina ya ujenzi wa jiji la Asman huko Issyk-Kul, na gharama ya mradi ilikadiriwa kuwa karibu dola bilioni 20, kulingana na takwimu kutoka Wizara ya Uchumi. Rais Japarov hapo awali alihusisha utekelezaji wa mradi huo na marekebisho yake na mahitaji ya mazingira.

Jarida la Ar-Raya: Mtego wa Ukraine na mustakabali wa NATO mipango ya kivita ya kuizunguka Urusi na kuizingira China

Jarida la Ar-Raya: Mtego wa Ukraine na mustakabali wa NATO mipango ya kivita ya kuizunguka Urusi na kuizingira China

Jumuiya ya kujihami ya Nchi za Magharibi (NATO) imeanza kuweka mipango ya kivita na tafiti za siku za usoni kuhusu vita kati yake na Urusi, na nchi za NATO zimepitisha na kuandaa "maelfu ya kurasa za mipango ya kijeshi" ambayo ilielezewa kuwa "ya siri", na zinazohusiana na makabiliano yanayowezekana na Moscow. Mipango hii inajumuisha maelezo ya makabiliano ya kijeshi yanayowezekana na Urusi kwa mara ya kwanza katika miongo kadhaa, na wataalamu wanasema: "Hii ni kwa sababu NATO, baada ya kuanza kwa vita vya Urusi dhidi ya Ukraine, ilikagua sera yake kuelekea Shirikisho la Urusi, ambalo haikuliona kwa muda mrefu kama tishio kubwa kwa muungano."

Jarida la Ar-Raya: Kulazimisha Ada kwa Maji ya Nile ni Ukiukaji wa Mali ya Umma na Ukiukwaji wa Wazi wa Hukumu ya Sharia

Jarida la Ar-Raya: Kulazimisha Ada kwa Maji ya Nile ni Ukiukaji wa Mali ya Umma na Ukiukwaji wa Wazi wa Hukumu ya Sharia

Jukwaa la Mazeed lilisema kwenye tovuti yake Ijumaa 2025/10/16, kwamba Waziri Mkuu wa Misri, Mustafa Madbouly, alitoa uamuzi mpya Na. 3744 wa mwaka 2025 kulazimisha ada za kifedha kwa matumizi ya maji ya Mto Nile na njia za maji na kuinua maji kwa madhumuni yasiyo ya kilimo, kwa kisingizio cha "usimamizi bora wa rasilimali za maji" na kukabiliana na upungufu wa maji. Uamuzi huo ulitolewa siku moja baada ya uamuzi mwingine kama huo, na ulikuwa na maandishi ya kukusanya ada ya kifedha kwa kila mita ya ujazo ya maji kulingana na madhumuni ambayo yanatumika, 

Jarida la Al-Raya: Yaliyofichika Katika Historia ya Yemen ya Kisasa

Jarida la Al-Raya: Yaliyofichika Katika Historia ya Yemen ya Kisasa

Katika miaka ya hivi karibuni, mifumo miwili mipya ya utawala ilianzishwa nchini Yemen; wa kwanza ukiwa Sana'a na wa pili Aden. Nani aliondolewa na nani alikuja? Wa kwanza alimuondoa mrithi wa Ukhalifa wa Ottoman, na akamwondoa kutoka madarakani huko Sana'a na kaskazini mwa Yemen - ambaye hakufikiria kuutumia ulimwengu uliostaarabika dhidi yake baada ya kuondolewa kwa Ukhalifa wa Ottoman kutoka eneo la kisiasa la kimataifa - na wale waliohusika na mfumo mpya wa utawala walielekeza akili zao kuelekea Magharibi, kuchukua kile ilicho nacho katika kupanga masuala mbalimbali ya maisha.

Jarida la Al-Raya: Makala Mbalimbali za Al-Raya – Toleo la 572

Jarida la Al-Raya: Makala Mbalimbali za Al-Raya – Toleo la 572

Hali ya watu wa Palestina haitengenei, wala hawaokolewi wala hawasaidiwi ila kwa msukumo wa jeshi la Kiislamu, na ila kwa mwito wa jihadi na nara za takbira, na msafara wa askari wakombozi, siku hiyo wataamini watu wa Gaza na utafurahi Msikiti wa Al-Aqsa na waliomo ndani yake huku wakitawala juu ya magofu ya viti vya enzi vya madhalimu, na hakika kheri hii na jukumu hili kuu halitafuatiliwa ila na yule aliyemtakasia Mwenyezi Mungu kutoka katika umma wa Kiislamu na jeshi lake, Mwenyezi Mungu awaongoze nyoyo zao na awafungulie vifua vyao kwa ajili ya kuinusuru dini yake, na hilo si gumu kwa Mwenyezi Mungu.

Dharau ya Marekani kwa Raia Wake Inawaacha Wanawake na Watoto na Njaa

Dharau ya Marekani kwa Raia Wake Inawaacha Wanawake na Watoto na Njaa

Mpango wa Msaada wa Lishe wa Ziada (SNAP) ni programu ya shirikisho inayosaidia watu binafsi na familia zenye kipato cha chini na watu wenye ulemavu kupata marupurupu ya kielektroniki yanayotumika kununua chakula na vinywaji, isipokuwa vileo, na mimea ya kujipandia chakula chao wenyewe. Ripoti zinaonyesha kuwa Wamarekani milioni 42 wanategemea marupurupu ya (SNAP) kujilisha wao na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea marupurupu ya chakula ni wanawake, wengi wao wakiwa mama wasio na waume, na 39% yao ni watoto,

Al-Khalil Habari: Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan Wakutana na Idadi ya Viongozi wa Mji wa Al-Abyad

Al-Khalil Habari: Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan Wakutana na Idadi ya Viongozi wa Mji wa Al-Abyad

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, jana Jumatatu, Novemba 3, 2025, ulizuru idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini, na ujumbe huo uliongozwa na Profesa Al-Nadhir Muhammad Hussein Abu Minhaj, mwanachama wa baraza la Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Profesa Muhammad Saeed Boukeh, wanachama wa Hizb ut-Tahrir.

21 / 10603