Hatimaye Majeshi Yetu Yataingia Palestina Lakini Siyo Kuyatakasa Kutoka Kwa Wayahudi Bali Kumtumikia Trump
Trump aliwakusanya wafuasi wake kutoka kwa watawala wa Kiislamu huko Cairo mnamo Oktoba 14, 2025 ili kujigamba kuhusu mafanikio yake katika kufikia makubaliano kuhusu Gaza. Mwandishi wa BBC katika Wizara ya Mambo ya Nje aliripoti mnamo Oktoba 10 kwamba "Marekani inahamisha hadi wanajeshi 200 ambao tayari wamewekwa Mashariki ya Kati hadi Israeli kuratibu operesheni hiyo, kulingana na maafisa wa Marekani. Jeshi la Marekani litaanzisha kile kinachoitwa kituo cha uratibu wa kiraia na kijeshi nchini Israeli, ambacho kitajumuisha karibu wanajeshi 200. Kitajumuisha vikosi kutoka nchi za Kiarabu na Kiislamu, ikiwa ni pamoja na Misri, Qatar na Uturuki".