Shambulio la Shirika la Kiyahudi dhidi ya Qatar Halipaswi Kusomwa Bila Kujali Sera ya Amerika Katika Eneo Hilo
Shambulio la shirika hilo dhidi ya Qatar halipaswi kusomwa bila kujali sera ya Amerika na mikakati yake ya kikoloni katika eneo hilo, kwa sababu Amerika ndiyo inayoshika nafasi ya uongozi katika ngazi ya kimataifa, na kwa hiyo, ndiyo yenye nguvu na ushawishi wa kisiasa ulimwenguni. ndiye mmiliki wa mfumo wa kimataifa, mifumo, taasisi na vyombo, kwani ndiye aliyeiunda na kuweka misingi yake baada ya Vita vya Pili vya Dunia, na ulimwengu leo unaenda kulingana na sheria zake, kwa hiyo Amerika hadi sasa ndiyo nchi ya kwanza katika kuchora sera za kimataifa na msimamo wa kimataifa.