Maombolezo ya Anas Al-Sharif na Wenzake
Katika jioni ya Jumapili, Agosti 10, 2025, hema ndogo ya habari mbele ya Jengo la Matibabu la Al-Shifa katika mji wa Gaza liliharibiwa kabisa na shambulio la moja kwa moja kutoka kwa chombo cha Kiyahudi, na kusababisha kuuawa shahidi kwa waandishi wa habari watano waliokuwa wakiandika mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza. Miongoni mwa mashahidi hao walikuwa waandishi wa habari Anas Al-Sharif, Mohammed Qurayqa, na wapiga picha Ibrahim Zaher, Moamen Aliwa, na Mohammed Nofal, Mwenyezi Mungu awarehemu na awakubali miongoni mwa manabii, wasadikifu, mashahidi, na watu wema, na hao ni rafiki wema.